Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

TAREHE RASMI YA KUANZA KWA MKUTANO WA KIMATAIFA WA OYES 2017 YAJULIKANA


Tarehe rasmi ya kuanza kwa mkutano mkubwa wa kitaifa na kimataifa wa OYES (Open your Eyes and See) 2017 unaoandaliwa kila mwaka na kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza imejulikana.

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa hilo, Dkt.Daniel Moses Kulola, amebainisha kwamba mkutano huo utaanza jumamosi Mei 27 na kufikia tamati jumapili Juni 04, 2017 katika viunga vya kanisa hilo vilivyopo nyuma ya Soko Kuu la Sabasaba Jijini Mwanza.

Kupitia BMG Habari, Dkt.Kulola amebainisha kwamba waimbaji na watumishi wa Mungu kutoka ndani na nje ya nchi akiwemo Mchungaji Gary White kutoka Amerika watahudumu katika mkutano huo.

Mafundisho pamoja na mahubiri ya neno la Mungu yaliyolenga kumfungua kila mmoja ili aone Ukuu wa Mungu yatafundishwa katika mkutano huo na kama ilivyo kawaida mamia ya wananchi wanatarajiwa kufunguliwa kwenye mkutano wa OYES 2017.
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO