Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

TASWIRA: COASTAL UNION YAIBANJUA OLJORO 2-0 JIJINI ARUSHA KATIKA MECHI ZA UFUNGUZI WA LIGI KUU YA VODACOM

                                         Kikosi cha leo hiki kilichoanza dhidi ya Oljoro JKT.

                         Yayo Kato akituliza mpira mbele ya Majaliwa Mbaga wa JKT Oljoro.

Mashabiki wa Coastal Union waliuteka uwanja wa Sheikh Amri Abeid leo. Watu wote mazungumzo ni kigoma hiki.

Yusuf Machogote wa JKT Oljoro akijaribu kukimbilia mpira na Suleiman Selembe leo.

Hiki ni kipindi cha pili Selembe alikosa bao la wazi yeye na golikipa. Na hili lilikuwa bao la pili kukosa baada ya kipindi cha kwanza kupewa pasi murua na Yayo akabaki na golikipa akapiga kichwa mpira ukatoka nje.

Uhuru Suleiman akijaribu kutafuta mbinu za kumtoka mchezaji wa Oljoro leo.

Selembe akimpongeza Abdi Banda baada ya kufunga bao la kwanza ndani ya dakika 16 ya mchezo.

Hapa Banda akiwa anarudi kutoka kufurahia na mashabiki wa Coastal Union waliofurika uwanjani leo.

Mwamuzi wa leo kutoka Mwanza Jacob Adengo akimwonyesha kadi ya Njano Banda kwa kutoka nje ya uwanja wakati mpira ukiendelea.

Shaaban Kado leo alikuwa nyota ya mchezo baada ya kuopoa michomo mingi ambayo iliyawacha watu mdomo wazi.

                                                 Morocco akisisitiza jambo uwanjani.

               Haruna Moshi Boban leo alivutia watu wengi kutokana na style yake ya kucheza.

Hamad 'Basmat' akikokota mpira bila wasiwasi wowote, leo alipiga beki nzuri hakuna mchezji aliyethubutu kumsogelea.

                                                Selembe akituliza mpira kwa ufundi mkubwa.

                         Haruna Moshi 'Boban' akituliza mpira mbele ya wachezaji wawili wa Oljoro.

              Mashabiki wa Coastal Union baada ya mpira kuisha ilikuwa raha tu mwanzo mwisho.

Nassor Binslum, Akida Machai na Heme Hilal wakiwa katika viunga vya jiji la Arusha baada ya mechi kuisha kwa ushindi 2-0.

Mwenyekiti wa Coastal Union Hemed Hilal 'Aurora' akisalimiana na Yayo Kato, kabla ya mpira kuanza.


PICHA ZOTE: http://coastalunionsc.blogspot.com


Matokeo kamili ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania kwa mechi za jana
Mtibwa Sugar 1 - 1 Azam FC
Rhino Rangers 2 - 2 Simba SC
Coastal Union 2 - 0 JKT Oljoro
Mbeya City 0 - 0 Kagera Sugar
Ruvu Shooting 3 - 0 Tanzania Prisons
Young Africans 5 - 1 Ashanti Unite

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO