Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Lema aanza ziara maalumu kufuatilia shughuli za maendeleo Jimboni kwake

Pichani ni mbunge wa Arusha Mjini kupitia Chadema, Mh Godbless Lema akihutubia mamia ya wakazi wa Kata ya Baraa katika mkutano wake leo jioni kufuatlia shughuli za maendeleo Jimboni kwake, hasa ujenzi wa Kituo cha afya cha katika Kata ya Baraa.


Wakati huo huo.. Diwani Mteule Kata ya Kaloleni amefanya mkutano wa kuwashukuru wananchi waliomchagua

Kamanda wa Chadema, Ally Bananga akiwashukuru wananchi wa Kaloleni kwa kuichagua Chadema Kata ya Kololeni katika uchaguzi uliofanyika Julai 14, 2013 na Chadema kuibuka washindi kwa tofauti kubwa ya kura dhidi ya CCM na CUF na kunyakua Kata zote nne zilizokuwa zinashindaniwa (Kaloleni, Kimandolu, Themi na Elerai)

Bananga katika hotuba yake, amemhusia Diwani wa mteule wa Kaloleni Mh Emmanuel Kessy kwa kumkumbusha kwamba Chadema ni chama chenye ujasiri wa kufanya maamuzi magumu kwa maslahi ya cham na taifa na hivyo kama atafanya mzaha na wajibu aliokabidhiwa kuwatumikia wananchi atashughulikiwa “Chadema ni chama cha maamuzi magumu ukileta mchezo tunakaka mti tunapanda mti”, amesema Ally Bananga

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO