Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Henry Kilewo na wenzake wafutiwa mashitaka ya ugaidi..

Taarifa ambazo Blog hii imezipata muda huu kutoka Tabora zinaeleza kuwa Mahakama Kuu Kanda ya Tabora imetoa maamuzi yake juu ya shauri la kesi ya ugaidi kwa washtakiwa, Henry John Kileo, Evodius Justian, Oscar Kaijage, Seif Kabuta na Rajab Kihawa kwa KUFUTA MASHTAKA YA UGAIDI dhidi yao.

kILEWO2Mke wa Katibu wa Chadema Kanda Maalumu ya dar es Salaam Henry Kilewo; Bi Joyce Kiria akiwa ndani ya chumba cha Mahakama kabla ya hukumu kutolewa

Kilewo3Picha ya Maktaba, watuhumiwa waliofutiwa mashitaka ambayo Chadema walieleza mkakati wake kabla hata hayatekelezwa

Kilewo5Henry Kilewo mwishoni ukutani akiwa na fikra nzito labda kwa kutokujua hatma ya hukumu dhidi yake na wenzake mapema leo

Kilewo4

Mke wa Henry Kilewo, Bi Joyce Kiria akiwa na tabasamu pana

PICHA ZOTE KWA HISANI YA JOYCE KIRIA


Jikumbushe
Maamuzi haya yanafuatia kesi hiyo ya rufaa ya jinai namba 53/2012 ilifunguliwa na Wakili wa Utetezi, Peter Kibatala na kuanza kusikilizwa Julai 22 mwaka huu mbele ya Jaji Lukelelwa ikiomba miongozo ya kisheria ikiwemo yaliyotolewa na mahakama za wilaya na mkoa.

Shauri la maombi ya marejeo liliwakilishwa na Wakili Peter Kibatala anayewatetea washitakiwa, akiiomba mahakama kuu ipitie majalada ya kesi mbili dhidi ya wateja wake zilizofunguliwa mahakama hizo baada ya kuona maamuzi yake hayakutenda haki.

Wakili Kibatala alibainisha katika maombi hayo kwamba kutokana na maamuzi hayo ya mahakama za chini yameathiri pia haki za waomba rufaa ikiwa ni pamoja na kuwanyima haki ya kupata dhamana.

Kwa upande wake Serikali ilishindwa kujibu maombi hayo, badala yake ilijenga hoja kwamba walichelewa kupata nyaraka hizo kwani walizipokea siku moja kabla ya kutajwa shauri hilo hivyo walishinda kuzijibu.

.Kilewo

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO