Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

UCHAGUZI UKIENDELEA ZIMBABWE: VYAMA VIWILI VYAMUUNGA MKONO MORGAN TSVANGIRAI

Vyama viwili vya  kisiasa nchini Zimbabwe vimemuunga mkono waziri mkuu Morgan Tsvangirai katika uchaguzi ujao wa urais.Vyama hivyo vimeahidi kuunda serikali ya umoja baada ya uchaguzi uliopangwa kufanyika Julai 31.

Jumapili, waziri wa fedha wa zamani na mshirika wa karibu wa zamani wa rais Robert Mugabe, Simba Makoni alisema kuwa  ameunda ‘ chama mseto cha mabadiliko' na waziri mkuu Morgan Tsvangirai na chama kingine cha kisiasa kwa lengo la kumshinda bw. Mugabe katika uchaguzi wa Julai 31.

Uamuzi wa vyama hivyo vya kisiasa kuunda ushirika huenda ulitokana na somo walilolipata kufuatia uchaguzi wa 2008 ambapo bw.Tsvangirai alishindwa kupata wingi wa kura katika duru ya kwanza ya uchaguzi. Katika uchaguzi huo bw. Makoni alipata asili mia 9 ya kura.

Jumapili, bw. Tsvangirai alisema atagombania urais Julai 31 licha ya kutoridhishwa na ukosefu wa mabadiliko ya kidemokrasia katika taifa hilo. Lakini wizara ya fedha ya Zimbabwe inasema itahitaji takriban dola milioni 132 kugharamia uchaguzi huo.

Waziri wa fedha bw. Tendai Biti anasema itambidi bw. Mugabe kuyasukuma makampuni ya migodi ya almasi kutoa fedha za mauzo ya madini hayo iwapo uchaguzi huo utaendelea. Uhcaguzi huo utaashiria kumalizika kwa serikali ya muungano baina ya bw. Mugabe na bw. Tsvangirai  iliyoundwa  baada ya uchaguzi wenye utata wa  2008.

Chanzo: Reuters

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO