Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Hotuba ya kwanza ya rais Obama tangu kuapishwa juu ya hali ya kitaifa; aahidi kufufua uchumi Marekani

Rais Barack Obama, akitoa hotuba ya hali ya kitaifa Feb. 12, 2013

Rais Barack Obama, akitoa hotuba ya hali ya kitaifa Feb. 12, 2013

Rais wa Marekani Barack Obama ametoa hotuba yake Jumanne usiku juu ya hali ya kitaifa. Mojawapo ya maswala aliyoyapa uzito yakiwa swala la uchumi na ajira. Akigusia moja ya mambo yenye utata  Bw. Obama alitoa wito tena kuwe na juhudi madhubuti za kufanya mabadiliko katika sheria juu ya umilikaji wa silaha.

Alisema  yale machache  aliyozungumzia  katika hotuba ya Jumanne usiku  yatakuwa muhimu ikiwa mabaraza ya bunge yatakubaliana kulinda kile alichosema ni raslimali muhimu sana -nao ni watoto. Pia aliwataka wabunge kupigia kura mswada wa kuchunguza  historian na tabia za  watu wanaonunua bunduki na kuondoa silaha za kijeshi mitaani ili kulinda maisha ya raia wa Marekani wanaoendelea kuuawa kiholela na watu wenye bunduki .

Ghasia za bunduki zimekuwa suala kubwa tangu mauaji ya halaiki ya mwezi Desemba ya katika shule ya watoto ya Sandyhook jimbo la Connecticut .

Rais Obama aliahidi tena kuhakikisha nafasi sawa kwa wanajeshi wote ikiwa ni pamoja na mafao kwa familia zao hata kwa wale wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja.

Amesema pia wanajeshi wa Marekani wataondoka Afghanistan kama ilivyopangwa mwaka wa 2014 na kwamba Marekani  ni taifa lenye  bora zaidi kuliko yote duniani.

Chanzo: Voice of America/Swahili

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO