Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Ghana, Nigeria zaing'arisha Afrika huko Brazil

Timu za Ghana na Nigeria kutoka Afrika zimefanikiwa kuitoa kimasomaso Afrika katika michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea nchini Brazil kwa Ghana kutoka sare ya goli 2.2 dhidi ya miamba ya Ujerumani na Nigeria kuwafunga goli 1 kwa bila katika mechi za usiku wa jana kuamkia leo.

Wajerumani hawakuamini kilichokuwa kikifanywa na vijana wa Ghana huku mshambuliaji wao Miloslav Klose kutokea benchi na kuisawazishia Ujerumani na yeye kufikisha goli 15 katika michuano ya kombe la Dunia, rekodi ambayo ilikuwa inadhikiliwa na Ronaldo De Lima wa Brazil.

Ndugu familia ya Boateng, Prince Boateng anyechezea Ghana kushoto na kaka yake Jerome Boateng anayechezea Ujerumani Miroslav Klose akiruka sarakasi kushangilia goli lake la 15 na la kuisawazishia Ujerumani katika michuano ya Kombe la Dunia. Dede Ayew akishangilia goli la kwanza alilofunga kwa Ghana Mtifuano uwanjani ********** Nigeria na ushindi wa kwanza katika miaka 16 Timu ya Nigeria ilifanikiwa kuifunga Bosnia&Herzegovina goli moja kwa bila kupitia mchezaji Peter Odemwingie na kuweka rekodi ya kushinda mechi ya kwanza katika miaka 16 ya kombe la Dunia. Peter Odemwengie akishangilia goli lake lililowaonfosha Bosnia kwenye michuano hiyo Wachezaji wa Nigeria wakimpongeza mwenzao Odemwengie kufunga goli lililovunja rekodi ya Nigeria kukosa ushindi kwenye Kombe la Dunia kwa takribani miaka 4. --- Picha zote na mitandao ya kimataifa.
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO