Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

KAMPUNI YA BIDHAA YAMCHANGANYA BARACK OBAMA NA CHRIS SMALLING KATIKA UTENGENEZAJI WA BIDHAA ZA KUHAMASISHA MASHABIKI TIMU YA UINGEREZA

Getty Images

KOMBE LA DUNIA 2014 NCHINI BRAZIL, Limekuwa si tu kombe la dunia la kusahau kabisa kuwazungumzia Uingereza dimbani kwa kusahau kama nao wanashiriki kombe hilo, bali pia limekuwa ni kombe ambalo hata baadhi ya makampuni yamepata ugumu kuweka picha sahihi za wachezaji wa timu hiyo ya taifa kwenye bidhaa za promosheni, kwani takwimu zinaonyesha wachezaji wa timu hiyo ya Uingereza hawajafanya lolote jipya ambalo lingeweza kuwafanya taswira zao kukaririka na kubakia vichwani mwa watu. 

Kampuni moja lililojikita katika utengenezaji wa thamani za majumbani ambalo linategemea kuvuna fedha nyingi kwa kuuza vikombe vya kunywea chai na kahawa vyenye picha za wachezaji wa timu za mataifa mbalimbali yanayo shiriki Kombe la Dunia ikiwemo timu ya Taifa ya Uingereza, limejikuta kwenye mkumbo huo wa kutobaini utofauti wa picha ya mchezaji Chris Smalling na ile ya Rais wa Marekani Barack Obama. Imebainika kupitia Gazeti la Sunday Express.

Unaweza kununua bila utata vikombe vya wachezaji kama Steven Gerrard or Joe Hart or Wayne Rooney na wengineo lakini utata unakuja pale utakapo kuwa shabiki wa Chris Smalling  na kuhitaji kikombe cha mchezaji huyo, utakutana na kitu cha utofauti na utastuka ukijiuliza maswali.. Jeh na huyu tena rais wa nchi nyingine ni mchezaji wa Uingereza?!!

Kikombe na utata:- Jina ni mchezaji husika timu ya taifa ya Uingereza, picha ni ya Rais wa Marekani Barack Obama.

Rais wa Marekani Barack Obama hachezi kama mtu wa kati kwa klabu ya  Manchester United na wala timu ya taifa ya Uingereza.

 

SHARED FROM G SENGO

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO