Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Polisi wa Ufaransa Matatani Kwa Ubaguzi Wa Rangi

POLISI WA UFARANSA MATATANI KWA
UBAGUZI WA RANGI
Mzozo wa ubaguzi wa rangi unatokota nchini
Ufaransa baada ya picha kupatikana za
maafisa wa polisi wazungu wakiwa wamejipaka
rangi nyeusi huku wakiiga mienendo ya nyani
katika sherehe moja.
Mkuu wa polisi wa Ufaransa ameanzisha
uchunguzi juu ya suala hilo, baada ya picha
hizo kupatikana katika ukurasa wa Facebook
wa afisa mmoja wa polisi, imeripoti tovuti ya
Channel 4.
Maafisa hao wa polisi wanadhaniwa ni kutoka
kikosi cha Kremlin-Bicêtre, kusini mwa Paris.
Hii si mara ya kwanza kwa polisi wa Ufaransa
kutuhumiwa kwa ubaguzi wa rangi katika
mitandao ya kijamii. Mwaka 2013 afisa mmoja
wa kike wa polisi alitoa maoni ya kibaguzi
hadharani.

Shared from Salim Kikeke's facebook page

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO