Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Ajali Moshono: Pick Up Hilux na Daladala Hiace zagongana uso kwa uso; Dereva wa Daladala kavunjikavunjika miguu yote

10299515_698921726813920_5029549875143891989_n

Ajali mbaya imetokea  maeneo ya Suye katika barabara ya Mandela ambapo gari ya abiria Hice yenye namba za usajili T…. inayofanya safari zake kati ya Nduruma na katikati ya Jiji imegonganga us kwa uso na Toyota Hilux double Cabin mapema sana asubuhi majira ya saa moja na nusu. Kwa mujibu wa mashuhuda, inaelezwa kuwa dereva Daladala maarufu kama ‘Vifodi”amevunjika vunjika vibaya miguu yote miwili.

Chanzo cha ajali kinaelezwa kusababishwa ulevi wa dereva wa Hilux ambaye alikua amelewa kiasi cha kuyumbayumba barabarani. Dereva huyo baada ya kusababisha ajali alijaribu kukimbia  na watu kumzuia, akatoa bastola yake na kuleta kizaazaa kikubwa eneo la tukio ambapo barabara ilikuwa imefungika kwa mda hivyo kusababisha umati mkubwa wa watu kushuka kwenye magari na kulizunguka eneo hilo. Hata hivyo Polisi waliwahikufika na kumdhibiti na hali ya utulivu ikarejea.

10277168_698921906813902_4994584036942244635_n

1544607_698921680147258_5401702979124901094_n

1538897_698921770147249_6331144358783336375_n

Picha zote na Emmanuel Lukwaro

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO