Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Bernard Membe Amkabidhi Rasmi Rais Jakaya Kikwete Tuzo ya Heshima ya Kiongozi Mwenye Mchango Mkubwa ziadi katika Maendeleo Barani Afrika kwa mwaka 2013

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akitoa maelezo mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete kabla ya kumkabidhi Tuzo ya Heshima ya Kiongozi Mwenye Mchango Mkubwa ziadi katika Maendeleo Barani Afrika kwa mwaka 2013 aliyoipokea kwa niaba ya Mhe. Rais Kikwete tarehe 9 Aprili, 2014 Jijini Washington D.C, Marekani. Heshima hiyo kwa Rais Kikwete ilitolewa na Jarida Maarufu la Kimataifa la African Leadership Magazine Group.

Mhe. Rais Kikwete na Wajumbe wengine waliokuwepo akiwemo Mkurugenzi wa Mawasiliano, Ikulu, Bw. Salvatory Rweyemamu wakimsikiliza Mhe. Membe.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akipokea toka kwa  Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membekupokea Tuzo ya Uongozi Bora Afrika aliyotuzwa nchini Marekani ambako aliwakilishwa na Mhe Membe.

Mhe. Membe akimkabidhi rasmi Mhe. Rais Kikwete Tuzo yake.

  Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe, wakiangalia cheti cha heshima alichopewa na Gavana wa Maryland wakati wa kupokea Tuzo ya Uongozi Bora Afrika aliyotuzwa nchini Marekani ambako aliwakilishwa na Mhe Membe.

Mhe. Rais Kikwete akionesha Tuzo hiyo mara baada ya kuipokea kutoka kwa Mhe. Membe.Picha na IKULU  na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO