Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

BASI LA URIO SAFARIS LAPINDUKA NA KUJERUHI 31 ENEO LA KIA

Basi la kampuni ya Urio Safaris lenye namba za usajili T 137 BCX inayofanya safari zake kati ya Moshi na Leguruki mkoani  Arusha leo limepinduka katika eneo la Kia na kujeruhi watu zaidi ya 31.


Kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwepo katika eneo la tukio walisema kuwa ajali hiyo ilitokea baada ya dereva wa basi hilo kujaribu kukwepa pikipiki iliyokuwa imeingia barabarani kwa ghafla.


"dereva huyu alikuwa anajaribu kukwepa pikipiki ndipo gari ikamshinda na kuhama barabara ndipo ilipo anguka gafla  na kubiringita mara tatu. Hapa yenyewe unavyoiyona tumeigeuza ilikuwa kichwa chini matairi juu" alisema mmoja wapo wa shuhuda ambaye akutaka kutaja jina


Mpakamtoa taaifa anaondoka eneo la tukio watu 31 walikuwa wamekwishwa pelekwa katika hospitali ya Wilaya ya Hai kwa ajili ya matibabu wakiwemo wanafunzi wa shule ya Leguruki ambao walikuwa wanarejea shuleni mara baada ya kumaliza likizo yao ya sikukuu ya Pasaka.

Wananchi wawakiwa wanashuhudia ajali hiyo iliotokea leo jioni katika eneo la kia ambapo inasemekana watu zaidi ya 31 wamejeruliwa

Picha ya chini na juu ni baadhi ya majeruhi walikuwa kwenye  basi hilo aina ya Urio lililopata ajali leo jioni katika eneo la Kia Wilayani Hai  mkoani Kilimanjaro




 

PICHA ZOTE NA: LIBENEKE LA KASKAZINI BLOGU

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO