Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Taswira Kutoka Waziri ya Fedha: Waziri Mkuya na Ujumbe wake wakutana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Afrika na uongozi wa mfuko Changamoto za Milenia.

 

Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum Mkuya wa katikati akiandika maelezo na hoja kutoka Mkurugenzi Mtendaji wa kundi la Afrika ( Afrika Group 1 Constituency)Bi.Chileshe Mpundu Kapwepwe(hayupo kwenye picha). kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile na kutoka kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya fedha Zanzibar Bw. Khamis Mussa na akifuatiwa na Gavana msaidizi wa Benki kuu ya Tanzania Bi. Natu Mwamba.

Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum Mkuya wa katikati akiwa pamoja na ujumbe kutoka Tanzania katika majadiliano na Mkurugenzi Mtendaji wa kundi la Afrika ( Afrikca Group 1 Constituency)Bi.Chileshe Mpundu Kapwepwe(hayupo kwenye picha). kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile akifuatiwa na Katibu Mtendaji Ofisi ya Rais Tume ya Mipango Dr. Philip Mpango.Kutoka kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya fedha Zanzibar Bw. Khamis Mussa na kufuatiwa na Gavana msaidizi wa Benki kuu ya Tanzania Bi. Natu Mwamba.Pamoja na ujumbe kutoka Tanzania.

Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum Mkuya akielezea jinsi Tanzania inavyotekeleza sera zilizowekwa na mashirika ya kimataifa kama (WB) na (IMF) kwa Mkurugenzi Mtendaji wa kundi la Afrika ( Afrikca Group Constituency)Bi.Chileshe Mpundu Kapwepwe.kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile.

Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum Mkuya akisikiliza kwa makini maswali aliyokuwa akiulizwa na Mkurugenzi Mtendaji wa kundi la Afrika ( Afrikca Group Constituency)Bi.Chileshe Mpundu Kapwepwe hayupo kwenye picha.Kulia kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile.

Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum Mkuya wa katikati akiwa pamoja na ujumbe kutoka Tanzania walipokutana na uongozi wa Mfuko wa Changamoto za Milenia (MCC) Kulia kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile na Bw. Ngosha Saidi Magonya, Kamishna wa Fedha za nje.Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Marekani – Washington Mhe.Liberata Mulamula, Katibu Mkuu Wizara ya fedha Zanzibar Bw. Khamis Mussa na Bw. Laston Msongole ambaye ni Mtendaji Mkuu wa mfuko wa milenia wa awamu ya pili.

Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum Mkuya wa katikati akisikiliza kwa makini maelezo na msimamo wa uongozi wa Mfuko wa Changamoto za Milenia (MCC) hawapokwenye picha.Kulia kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile na kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Marekani – Washington DC. Mhe.Liberata Mulamula

CREDIT: VINAJA NA MATUKIO.COM

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO