Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

KATIBU BAWACHA TAIFA BI GRACE TENDEGA AWAAMBIA WAMAMA WA ARUSHA “IMETOSHA KUWA WAPINZANI, UCHAGUZI HUU TUNAINGIA IKULU, UWEZO TUNAO NA WATANZAIA WAMETUAMINI”

DSC_1163

DSC_1166

DSC_1173

Katibu wa BAWACHA Taifa Mh Grace Tendega akihutubia katika Mkutano Mkuu wa BAWACHA Jimbo la Arusha Mjini ambapo alikuwa mgeni rasmi. Mh Tendega amewaambia wanawake wenzake kuwa mwaka huu ni mwaka wa mwisho kwa chama chake CHADEMA kuwa wapinzani kwasababu wamejipanga kuhakikisha wanashinda katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba baadae mwaka huu na kukabidhiwa dola kwa mara ya kwanza.

Katibu huyo ambaye alizindua vazi rasmi la BAWACHA Arusha Mjini katika mkutano huo, aliwaeleza wanawake wenzake wa CHADEMA kuwa wana kila sababu ya kushinda uchaguzi huu kwasababu watanzania wako tayari kwa mabadiliko na kwamba kinachohitajika ni kuwahamasisha zaidi.

Mh Tendega aliwataka wanawake hao kuwashawishi wanawake wenzao wanaoweza kuwa viongozi na wanakubalika na jamii washiriki kuogombea nafasi mbali mbali za uongozi katika uchaguzi huu. Akisisitiza zaidi aliwatahadharisha kuwa ushindi huo haotokuja tu bila kujiandikisha na hivyo akawataka kuhamsisha wananchi kujinadikasha kwa wingi iwezekanavyo pindi zoezi la uandikishaji litakapowafikia ijapokuwa alidai NEC inabahatisha  tarehe zake.

Aidha, alitumia nafasi hiyo aliyopata kuhutubia kuwashukuru watu wa Arusha ambao alidai walisaidia kwa kiasi kikubwa katika kampenzi za uchaguzi mdogo wa Kalenga mwaka jana na kuwasihi wasichoke kuendelea kuhamasisha na maeneo mengine.

Akimzungumzia Mbunge wa Arusha Mjini Mh Godbless Lema, Mh Tendega alidai kuwa wao mikoani wanamtambua kama mbunge wa Taifa na sio wa Arusha pekee.

 

DSC_1106

DSC_1130

Wamama wa BAWACHA wakiserebuka kumuunga mkono mwanamama mwenzao aliyetambulisha nyimbo zake

DSC_1141

Mratibu wa BAWACHA Mkoa wa Arusha Mh Cecy Ndossi

DSC_1147

DSC_1150

Viongozi wa BAWACHA Jimbo la Arusha Mjini

DSC_1151

Mke wa Mbunge wa Arusha Mjini Bi Neema Lema akifuatilia yanayojiri mkutanoni

DSC_1154

Wamama wakiwa wamependeza na mavazi yao maridadi yenye nakshinakshi ya rangi za Chadema

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO