Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

VIONGOZI WASHIRIKI KWA WINGI KUTOA HESHIMA YA MWISHO KWA MWILI WA JOHN NYERERE

Katibu Mkuu wa CHADEMA Dk Wilbrod Slaa alipozuru nyumbani kwa wafiwa kuwafariji. Picha za Dk Slaa Na: Chadema Blog

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoa heshima za mwisho mbele ya Jeneza lenye mwili wa marehemu John  

Nyerere, wakati wa shughuli za kuaga mwili huo zilizofanyika nyumbani kwa Mama Maria Nyerere Msasani, jijini Dar es Salaam leo Mei 11, 2015. Marehemu John 

anatarajia kuzikwa keshokutwa nyumbani kwao Butiama. Picha na OMR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwafariji wanafamilia baada ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa 

marehemu John Nyerere, wakati wa shughuli za kuaga mwili huo zilizofanyika nyumbani kwa Mama Maria Nyerere Msasani, jijini Dar es Salaam leo Mei 11, 2015. 

Marehemu John anatarajia kuzikwa keshokutwa nyumbani kwao Butiama. Picha na OMR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na baadhi ya viongozi na waombolezaji nyumbani kwa Mama Maria 

Nyerere Msasani jijini Dar es Salaam, leo wakati wa shughuli za kuaga mwili wa marehemu John Nyerere. Marehemu John anatarajia kuzikwa keshokutwa nyumbani 

kwao Butiama. Picha na OMR

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Nape Nnauye akizungumza na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dk.Wilbroad Slaa wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa marehemu John Nyerere.

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano Mama Salma Kikwete akisaini kitabu cha rambi rambi kwenye msiba wa John Nyerere

Makama Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula akizungumza na Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba kwenye msiba wa John Nyerere .

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Rais wa awamu ya tatu Benjamini Mkapa kwenye msiba wa John Nyerere ambapo viongozi mbali mbali walijumuika kutoa heshima za mwisho.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda akimuonyesha jambo Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara)Philip Mangula kwenye msiba wa John Nyerere ,msasani jijini Dar es salaam.(Picha na Adam Mzee)

Makongoro Nyerere akisoma wasifu wa Marehemu John Nyerere

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitoa heshima ya mwisho kwa mwili wa marehemu John Nyerere.

PICHA HIZI NA MAELEZO KWA HISNI YA CCMCHAMA BLOG

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO