Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Lowassa Achangisha Mil 234 katika Harambee ya Msikiti wa Patandi Tengeru leo, Mbunge Lema achangia Mil 1

Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli Mh. Edward Lowassa amechangisha jumla ya shilingi millioni 234 katika Harambee ya kuchangia ujenzi wa Msikiti wa Patandi uliopo wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha ambayo  awali ilitangazwa kuwa mgeni Rasmi katika Harambee hiyo angekuwa Mheshimiwa Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyepata udhuru na badala yaek ndio Edward Lowassa akamuwakilisha. Fedha hizo ni pamoja na fedha taslimu na ahadi.

Katika Harambee hiyo, Mbunge wa Arusha Mjini Mh. Godlbess Lema kupitia tiketi ya CHADEMA amechangia jumla ya shilingi milioni 1 kusaidia ujenzi wa msikiti huo.

Msikiti wa Patandi upo katika eneo wanalokaa wananchi wenye imani mbalimbali na waumini wanaoutumia msikiti huo, na wamekuwa wakijitoa kwa namna nyingi katika kusaidia kujenga mshikamano baina ya jamii zinazowazunguka bila kuwa na vikwazo na pia wamekuwa wakishiriki katika kuwasaidia watoto yatima na wengine wenye uhitaji katika kukabiliana na maisha yao.

 Lowassa Patandi3

Mh Lowassa akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Msikiti wa Patandi

Lowassa Patandi

Lowassa Patandi1

Lowassa Patandi2

 
Picha : Kwa Hisani ya Mussa Abdallah, Arusha
 

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO