Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

TASWIRA MKUTANO WA UKAWA ARUSHA: KAFULILA, LISSU NA LEMA WATIKISA JIJI; PAMOJA NA MVUA KUBWA WANANCHI WAGOMA KUONDOKA UWANJANI

DSC_0658

Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA ambaye pia ni mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Mh Tundu Lissu akihutubia umati mkubwa wa wakazi wa Jiji la Arusha katika viwanja vya Shule ya Msingi Ngarenaro katika mkutano uliokuwa katika sura ya UKAWA kwa kuwashirikisha NCCR Mageuzi.

Mkutano huo nusura uathiriwe na mvua kubwa iliyonyesha wakati Mbunge wa Kigoma Kusini Mh David Kafulila akihutubia lakini mapenzi ya wafuasi wa CHADEMA kwa chama na viongozi wao yaliwafanya wavumilie kunyeshewa mpaka mwisho. Viongozi walikataa kukingwa na mvua hiyo na kujikuta wote wakilowa mwili mzima kama wananchi wengine.

Katika hotuba yake, Mh Lissu aliwaeleza wakazi wa Arusha kitendo cha Serikali ya CCM kukorofishana na karibu kila kundi la jamii kwa kutaja wafanyabiashara, walimu, madaktari, madereva, wafanyakazi n.k ni ishara kuwa chama hicho kimechokwa na kinaweza kuondoka madarakani katika Uchaguzi wa mwaka huu ambao alisisitiza ni lazima ufanyike mwaka huu.

DSC_0721 

Msafara wa Viongozi wa UKAWA. Kutoka Kushoto Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema, Mbunge wa Singida Mashariki Mh Tundu Lissu, Mbunge wa Kigoma Kusini Mh David Kafulila, Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa Patrobas Katambi na mwanausalama wa CHADEMA

DSC_0657

DSC_0602

Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR Mageuzi), Mh David Kafulila ambaye kwa siku za karibuni amejizolea sifa lukuki kwa kuweza kuanzisha sakata la ESCROW na kulisimamia mpaka mwisho bila kuhofia vitisho mbalimbali. Katika mkutano huo Kafulila aliwashukuru wakazi wa Arusha kwa mapokezi mazuri na kusisitiza kuwa anajisikia furaha sana kuhutubia umati mkubwa Jijini hapa ambapo ni mji wa kihistoria katika harakati nyingi za kisiasa nchini. Kafulila aliwataka wakazi wa Arusha kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura na kwamba wawe na imani kupitia UKAWA na kwa kura zao wataweza kuitoa CCM madarakani.

DSC_0550

Mwenyekiti wa Baraza la Vinaja CHADEMA Taifa Mh Patrobas Paschal Katambi akihutubia mkutanoni hapo ambapo aliataka vijana kutokubali kuyumbishwa na wanasiasa wanaojaribu kuupotosha umma kuhusu ushirikiano wa vyama vinavyounda umoja wa UKAWA. Katambi alisisitiza zaidi kwa kutolea mfano wa ziara waliyonayo kwa pamoja na Mbunge Kafulila kuzunguka mikoa ya Kaskazini. Pia aliwataka vijana kuwatayari wakati wowote kupinga jaribio lolote la Serikali kuongeza muda wa kufanyika Uchaguzi Mkuu tofauti na mwaka huu.

DSC_0583

Mh Godbless Lema akizungumza na wananchi wake hii leo ambapo alitumia muda mwingi kuwatoa hofu dhidi ya propaganda zilizoeneo Jijini hapa kwamba hatagombea Arusha Mjini tena na kwamba Jimbo la Arusha Mjini litarudi CCM. Lema aliwaambia wazipuuze propaganda hizo na kuziita ni za kipuuzi kwasababu hakuna namna ambayo CCM inaweza tena kuwashawishi wananchi wa Arusha kuichagua. Alisisitiza kuwa kwa muda mfupi aliowatumikia mbali na vikwazo vingi ameweza kutimiza wajibu wake kama mbunge kwa kiwango kikubwa huku akiorodhesha mambo mablimbali aliyotimiza kwa yeye binafsi na mengine kupitia madiwani wake.

Kwa pamoja, Mh David Kafulila na Mh Tundu Lissu walimuombea Mbunge Lema ruhusa kwa wananchi wa Arusha ili mbunge wao aendelee kufanya kazi ya siasa maeneo mengine nchini kuharakisha kile alichokiita ukombozi wa mara ya pili, na kwamba wasijikisike vibaya ama kudhani mbunge hakai nao Jimboni.

DSC_0499

Waheshimiwa Kafulila na Lissu wakipokelewa na Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Arusha, Kalist Lazaro mwenye tisheti)

DSC_0504

Viongozi wa CHADEMa na UKAWA wakiimba wimbo wa Taifa sambamba na wananchi (hawaonekani pichani) kabla ya kuanza hotuba zao

DSC_0517

Kutoka kushoto waliokaa Mh Godbless Lema, Mh Tundu Lissu, Mh David Kafulila, Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Arusha Mh Kalist Lazaro na Mwenyekiti CHADEMA Wilaya ya Arusha Mjini Derick Magoma

DSC_0526

Mh Kafulila akiteta jambo na Mh Lissu huku Mh Lema naye akiteta jambo na Mwenyekiti wa Vijana Arusha Mjini Mh Innocent Kisanyage

DSC_0555

Mama na mwanae akiendelea kufuailia mkutano huku akisaidiwa kukingwa mvua

DSC_0567

Mwenyekiti wa Vijana CHADEMA, Patrobas Katambi akisalimia wakazi wa Arusha waliojitokeza mkutanoni hapo baada ya kutambulishwa na Mbunge wa Arusha Mjini Mh Godbless Lema

DSC_0571

DSC_0591

Mh Kafulila akitamulishwa Jukwaani

DSC_0601

Wananchi wakiuatilia mkutano huku mvua ikiendelea kunyesha

DSC_0625

Mh Kafulila akisalimiana na Katibu wa CHADEMA Arusha Mjini Mh Lewis Kopwe. Wanaonekana walivyolowa chapa chapa

DSC_0629

Wananchi wamelowa lakini hawaondoki mkutanoni

DSC_0633

Mh Lissu akiwa amelowa mwili mzima na bado anaendelea kuhutubia huku mvua inayesha

DSC_0646

DSC_0663

Kutoka kushoto; Kalisti Lazaro, Patrobas Katambi, David Kafulila, Godbess Lema, Derck Magoma

DSC_0667

DSC_0669

Mwenyekiti na Katibu wa CHADEMA Arusha Mjini wakifurahia jambo

DSC_0678

Mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa (CHADEMA) ambaye pia ni mtangaza nia ya Ubunge Jimbo la Same Magharibi, Kamanda Chritopher Mbajo akiteta na Mwenyekiti wa Vijana CHADEMA Taifa Bw Patrobas Patambi, mwenye kombati

DSC_0691

Mtia nia wa Jimbo la Mkalama Singida, Kamanda George Gunda (mwenye kombati nyeusi) kwa pamoja na viongozi wengine wakifuatilia hotuba ya Mh Tundu Lissu (haonekani pichani)

DSC_0695

Mh Lema akiwatambulishwa viongozi wa Kata ya Ngarenaro na kueleza namna walivyoingilia kati hujuma ya kuchimbua uwanja huo mkutano usifanyike. Yupo diwani Doita

DSC_0714

Msafara wa viongozi ukuindoka uwanjani hapo mara baada ya mkutano kumalizika. Wananchi waliwazonga kiasi cha kusababisha kazi ya ziada kwa wanausalama.

DSC_0726

Eneo la uwanja wa Ngarenaro ambalo linadaiwa kupitishwa greda na wanaodhaniwa kuwa watu wa pinzani wa CHADEMA Jijini hapa kwa nia ya kujaribu kuzuia mkutano huu wa leo usifanyike eneo hilo, jaribio ambalo halikufua dafu kwani watu waliyapanda matuta hayo kama vile hakuna kitu na mwishowe kusawazika kiasi.

DSC_0681

Bossi Mzito wa Blog Hii Akiteta Jambo naMwenyekiti wa BAVICHA Patrobas Katambi

PICHA ZOTE NA SERIAJr NA MAKABAYO

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO