Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Abambwa Akitapeli Kwa Kujifanya Afisa Ushuru wa Jiji la Arusha, Apewa Mkongoto na Kukabidhiwa Polisi

Pichani ni mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la Ibrahimu Kafimbi, anyedaiwa kufanya utapeli kwa kujifanya afisa ushuru wa mabango ya Halmashauri ya Jiji la Arusha akiwa na pingu baada ya kukamatwa na kufikishwa kituo kikuu cha Polisi Arusha. 

Bwana Kafimbi anadaiwa kuwa kwa muda mrefu amekuwa akiwatapeli watu mbalimbali kwa kujifanya afisa ushuru wa mabango huku akichukua fedha na kutoa risiti feki isivyo halali, hadi alipowekewa mtego na kukamatwa hii leo.

 Hapa anaonekana akiwa mwenye majonzi baada ya kupewa kichapo wakati akikaidi kufikishwa kituoni
Hapa anaonekana akiomba asipigwe baada ya kuwekwa kizuizini

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO