Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Diwani wa Osunyai, Elirehema Nnko (CHADEMA) Aunda Kamati ya Wazazi kubuni Mikakati ya Elimu Bure isiyo Bure katika Kata yake

Diwani wa Kata ya Osunyai ya Jijini Arusha, Mh Elirehema Nnko (pichani kulia) akizugumza na wazazi na wananchi katika kikao cha mkakati kufanikisha sera ya Elimu Bure inafanikiwa kwa matokeo chanya ingawa sera hiyo inakabiliwa na changamoto kadhaa katika utekelezaji wake. 

Kikao hicho cha wazi kilifanyikia Shule ya Sekondari ya Sombetini ambapo kwa pamoja na wazazi hao walikubaliana kuunda kamati ya Wazazi yenye wajumbe 10 ambayo itafuatilia na kubuni mikakati itakayohakikisha ufaulu wa wanafunzi unakuwa wa kuridhisha na itakapolazimu watoto wale shuleni.

Akifananua zaidi, Nnko amesema lengo la kamati hiyo ya wazazi waliyoichagua ni kuhakikisha elimu bure haiwi bure kweli kwa maana ya watoto kumaliza shule bila kuwa na ufaulu na maarifa yanayotakiwa.


Aidha, Diwani huyo aliwahimiza  viongozi wenzake kushirikiana kwa mbinu na mikakati katika kutatua kero na changamoto zinazowakabili wananchi waliowaamini na kuwachagua kuwa viongozi wao.


 Sehemu ya wananchi waliojitokeza katika mkutano huo wa wazi kujadili mustakabali wa elimu ya watoto wao


  
Pichani ni Diwani wa Kata ya Olasiti ya Jijini Arusha pia, Mh Alex Marti katika kutano mwingine wa wazi kuhusu mjadala wa Elimu Bure na changamoto zake na namna ya kuzitatua katika Kata ya Olasiti.

Baraza la Halmashauri ya Jiji la Arusha linaundwa na madiwani 24 wa kuchaguliwa kutoka Chama cha Demokrasia (CHADEMA) na Maendeleo na mmoja kutoka CCM ambaye ni Diwani wa Kata ya Kati, Mh Tojo. Pia wabunge  wawili (mmoja wa kuchaguliwa Jimboni) na madiwani 8 wa viti maalumu kutoka CHADEMA


Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO