Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

RAIS MAGUFULI ATEUA MAKATIBU TAWALA MIKOA LEO. ORODHA KAMILI IKO HAPA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 25 Aprili, 2016 amefanya uteuzi wa Makatibu Tawala wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara.

Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa kati ya Makatibu tawala hao 10 ni wapya, 2 wamebadilishiwa vituo vya kazi na 13 wamebakisha katika vituo vyao vya sasa.

Makatibu Tawala wapya walioteuliwa ni kama ifuatavyo;
    1.Arusha -    Richard Kwitega
    2.Geita -      Selestine Muhochi Gesimba
    3.Kagera -     Armatus C. Msole
    4.Kilimanjaro -     Eng. Aisha Amour
    5.Pwani -      Zuberi Mhina Samataba
    6.Shinyanga -   Albert Gabriel Msovela
    7.Singida -     Dr. Angelina Mageni Lutambi
    8.Simiyu -    Jumanne Abdallah Sagini
    9.Tabora -   Dkt. Thea Medard Ntara
   10.Tanga -    Eng. Zena Said


Makatibu Tawala waliobadilishwa vituo vya kazi ni kama ifuatavyo;
1.Kigoma -   Charles Amos Pallangyo (Kutoka Mkoa wa Geita)
2.Morogoro -  Dkt. John S. Ndunguru (Kutoka Mkoa wa Kigoma)


Makatibu Tawala waliobakishwa katika vituo vyao vya sasa vya kazi ni kama ifuatavyo;
    1.Dar es salaam -  Theresia Louis Mbando
    2.Dodoma -     Rehema Hussein Madenge
   3. Iringa -   Wamoja Ayubu Dickolagwa
    4.Katavi -    CP Paul Chagonja
    5.Lindi -   Ramadhan Habibu Kaswa
    6.Mara -   Benedict Richard Ole Kuyan
    7.Manyara -     Eliakimu Chacha Maswi
    8.Mbeya-    Mariam Amri Mjunguja
    9.Mtwara -    Alfred Cosmas Luanda
   10.Mwanza -  CP. Clodwing Mathew Mtweve
   11.Njombe -   Jackson Lesika Saitabau
   12.Rukwa -   Symthies Emmanuel Pangisa
   13.Ruvuma -   Hassan Mpali Bendeyeko


Makatibu Tawala wa Mikoa 10 ambao wameteuliwa kwa mara ya kwanza, wataapishwa siku ya Jumatano tarehe 27 Aprili, 2016 saa tatu asubuhi Ikulu Jijini Dar es salaam.


Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam

25 Aprili, 2016
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO