Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MWANAHABARI MTOTO NA MWANAMAZINGIRA WA UN, GETRUDE CLEMENT AWASILI JIJINI MWANZA.


Shujaa Wetu, Mwanahabari Mtoto, Mwanamazingira Balozi wa Umoja wa Mataifa UN kutoka Mwanza Tz, Getrude Clement (16) jana amewasili nyumbani Jijini Mwanza majira ya saa tatu usiku na kupokelewa kwa shangwe na ndugu, jamaa na marafiki katika Uwanja wa Ndege Mwanza.

Alihudhuria Mkutano wa Umoja wa Mataifa nchini Marekani uliohusu Mabadiliko ya Tabia nchi (Climate Change) ambapo alihutubia õakiwakilisha kundi la Watoto na Vijana duniani.

Kutoka Kushoto Pichani ni Brightius Titus ambae ni Katibu wa Mtandao wa Watoto na Vijana Mkoani Mwanza MYCN, Katikati ni Getrude mmoja wa Watoto wa Mtandao huo na Kulia ni Shaban Magana ambae ni Mwenyekiti wa MYCN.

"Kitu ambacho nimejifunza ni kupata kujiamini zaidi kwa sababu ule Mkutano ulihudhuriwa na watu wengi, wakiwepo viongozi kutoka zaidi ya nchi 170 wanachama wa Umoja wa Mataifa. Wameniasa kusoma zaidi ili kufikia malengo yangu ambapo nitaendelea kuzungumza na wananchi pamoja na viongozi wao juu ya masuala ya mabadiliko ya tabia nchi ambapo nitakuwa balozi wao". Alisema Getrude.
"Wazazi wawaruhusu watoto wao katika kushiriki shughuli mbalimbali za vikundi ili waweze kujiamini zaidi katika kufikia ndoto zao". Anasema Mtoto Mwanahabari Getrude.
Shabani Njia (Kulia) ambae ni Mwenyekiti wa Mtandao wa Vijana na Watoto Mkoani Mwanza MYCN akizungumzia mapokezi ya Mwanahabari na Balozi wa Mazingira wa Umoja wa Mataifa akiwakilisha kundi la Watoto na Vijana Getrude Clement
Clement Leon ambae ni baba mzazi wa Getrude akizungumzia mapokezi ya mwanae katika Uwanja wa ndege Mwanza.
Rizik Athman ambae ni mzazi wa Getrude akizungumzia mapokezi ya mwanae katika Uwanja wa ndege Mwanza ambapo anafurahishwa na hamasa aliyonayo mtoto wake ikiwemo kujiamini katika masuala mbalimbali ikiwemo ya habari.
Getrude (Katikati) akiwa na Wazazi wake, Clement Leon (Kushoto) pamoja na Rizik Athman (Kulia).
Ndugu, Jamaa, Marafiki pamoja na Viongozi wa MYCN, mapema wakifurahia jambo wakati wakimsubiria Getrude
Ndugu, Jamaa, Marafiki pamoja na Viongozi wa MYCN wakiwa pamoja na Getrude.
Ndugu, Jamaa, Marafiki pamoja na Viongozi wa MYCN, wakifurahia na Getrude katika picha ya pamoja.
Mapokezi ya Mtoto Getrude
Mapokezi ya Mtoto Getrude
Mapokezi ya Mtoto Getrude, Wengi walimsubiria kwa hamu kubwa.
Shuja, Mwanahabari Mtoto, Mwanamazingira Balozi wa UN Getrude Clement baada ya kuwasili Jijini Mwanza.
Tazama HAPA Getrude akihutubia katika Mkutano wa UN
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO