Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

TASWIRA: RAIS MAGUFULI ALIPOKUTANA NA WENYEVITI NA MAKATIBU WA CCM WA WILAYA NA MIKOA DAR ES SALAAM LEO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akizungumza na Viongozi wa mikoa na wilaya wa Chama Cha Mapinduzi kutoka Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar ambapo aliwashukuru kwa kazi nzuri waliofanya kipindi cha uchaguzi na kuwataka kuwa wamoja na kukiimarisha Chama.
Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Mhe.Philip Mangula akizungumza na kutoa neno la shukrani kwa niaba ya Viongozi wote wa CCM waliofanikisha ushindi wa Chama.

Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan akitoa neno la shukran kwa wenyeviti na makatibu wa mikoa pamoja na wilaya walioshiriki kufanikisha ushindi kwa CCM

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza nwa Wenyeviti na Makatibu wa Chama wa mikoa na wilaya wa CCM ambao walioshiriki na kufanikisha ushindi kwa Chama Cha Mapinduzi.

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Mhe. Nape Nnauye akizungumza wakati wa kuwashukuru viongozi wa Chama waliofanikisha ushindi kwa CCM.

Baadhi ya Viongozi wa CCM wakinyoosha vidole kutaka kutoa maoni yao kwa Rais Magufuli.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Nachingwea Mhe. Albert Mnali akichangia maoni yake kwenye mkutano wa viongozi wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

PICHA NA MATUKIO ZAIDI
BOFYA HAPA
CREDIT: ADAM MZEE
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO