Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

KOCHA SYLVESTER MASH AFARIKI DUNIA

Enzi za uhai wake Marehemu Syvester Mash (kushoto) akipewa maelekezo toka kwa aliyekuwa kocha wa timu ya Tanzania Taifa Stars Kim Poulsen

G SENGO KUTOKA MWANZA ANARIPOTI KUWA….
Aliyekuwa Kocha Msaidizi wa Taifa Stars, Sylvester Marsh amefariki dunia alfajiri ya leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ambako ndiko alikuwa amelazwa akipatiwa matibabu.
Kwa mujibu wa Katibu mkuu wa Chama cha soka mkoawa Mwanza MZFA Nasib Mabrouk amethibitisha kutokea kwa msiba huo akisema kuwa ni kipindi zaidi ya mwaka sasa kocha Marsh amekuwa akiugulia na sasa Mwenyezi Mungu ameamua kumpumzisha hivyo amewataka wapenzi wa soka kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu huku akisema kuwa wasubiri taratibu za mazishi na harakati mbalimbali ambazo zitatangazwa baadaye leo mara baada ya kukamilika kwa taarifa kamili.
R.I.P SYLVESTER MASH

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO