Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

WAKAZI 10000 KUNUFAIKA NA UKARABATI BWAWA LA KALEMAWE

unnamed

Mshehereshaji wa kongamano la siku moja lililofanyika jijini Dar kuzungumzia ukarabati na uendeshaji wa bwawa la Kalemawe lililopo wilayani Same mkoani Kilimanjaro, Mtaalamu wa masuala ya fedha wa UNCDF, Bw. Imanuel Muro akisherehesha kongamano hilo. Katikati ni mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Same, Herman Kapufi akifuatiwa na Mkuu wa ushauri wa ufundi wa Mfuko wa Umoja wa mataifa wa Ukuzaji Mitaji (UNCDF), Bw.  Peter Malika.(Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog)

 

Na  Mwandishi Wetu

ZAIDI ya watu  10,000 wanaozunguka bwawa la Kalemawe wilayani Same mkoani Kilimanjaro watanufaika na  ukarabati wa bwawa hilo na kuwekewa muundo mpya wa kiutawala  na Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Ukuzaji wa Mitaji  (UNCDF).

Bwawa hilo ambalo lipo katika kata za Kalemawe na Ndungu lilijengwa na watawala wa Kiingereza mwaka 1952-1959  kwa ajili ya kusaidia shughuli za kilimo na ufugaji  baada ya kuanzishwa kwa hifadhi ya Mkomazi na hivyo wakazi kuzuiwa kwenda katika hifadhi hiyo kwa shughuli mbalimbali.

Taarifa ya kuwepo kwa mradi huo mkubwa, imetolewa na Mkuu wa ushauri wa ufundi wa Mfuko wa Umoja wa mataifa wa Ukuzaji Mitaji (UNCDF) nchini, Bw. Peter Malika wakati akiwakaribisha madiwani wa kata hizo ambao wameitwa katika kongamano la siku moja Dar es salaam kuzungumzia ukarabati na uendeshaji wa bwawa hilo.

DSC_0038

Pichani juu na chini ni Mkuu wa ushauri wa ufundi wa Mfuko wa Umoja wa mataifa wa Ukuzaji Mitaji (UNCDF), Bw.  Peter Malika (kulia) akizungumza machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Same, Herman Kapufi kufungua rasmi kongamano hilo.

Malika amesema Mfuko huo wa ukuzaji wa mitaji unasaidia ukarabati wa bwawa hilo kupitia mpango wake wa uendelezaji rasilimali kwa kutumia fedha za ndani (LFI) .

Amesema baada ya ukarabati huo,  mradi utaendeshwa kwa pamoja kati ya serikali na watu binafsi.

Malika alisema ukarabati huo unakidhi lengo la mfuko ambalo ni kuwezesha miundombini inayoleta maendeleo.

“Ukarabati na hatimaye uendeshaji wa bwawa hilo kutasaidia kuleta mabadiliko makubwa ya maendeleo ya mitaji kwa watu binafsi na umma.” alisema

DSC_0026

Kongamano hilo lililofunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Same, Herman Kapufi  lilizungumzia masuala ya umiliki, masuala ya kisheria ya taasisi, utawala bora, masuala ya kiufundi ya ukarabati,uvuvi wa samaki wa kibiashara, matumizi ya maji kwa ajili ya umwagiliaji, ufugaji, mabadiliko ya tabia nchi na mazingira, uwezeshaji kiuchumi kwa wanawake, mfumo wa utoaji wa huduma za fedha na masuala mengi mengine ya mipango ya maendeleo endelevu.

Kapufi alisema kwamba pamoja na kushukuru Mfuko wa Mitaji kukubali kuwasaidia, amesema bwawa hilo ni muhimu sana katika kuondoa migogoro na migongano ndani ya jamii pia na mamlaka ya hifadhi ya Mkomazi.

Alisema kurejeshwa kwa hali yake ya zamani kutasaidia wafugaji, wakulima na watumiaji wengine wa bawawa hilo  kama wavuvi wa samaki kila mmoja kuwa na nafasi katika matumizi ya bwawa.

DSC_0067

Mkuu wa wilaya ya Same, Herman Kapufi akizungumza kwenye kongamano la siku moja lililofanyika jijini Dar kuzungumzia ukarabati na uendeshaji wa bwawa la Kalemawe lililopo wilayani Same mkoani Kilimanjaro lililoandaliwa na UNCDF.

Aidha alisema ukarabati utakaofanywa na muundo wa uendeshaji wa bwawa hilo utasaidia wilaya pia kufikiria namna ya kutengeneza bwawa jingine katika Mto Ruvu kwa sababu kama hizo za kuwapa uwezo zaidi wananchi katika maendeleo yao kwa kutumia rasilimali maji.

Toka kujengwa kwake katika miaka ya 1950, bwawa hilo lenye urefu wa takaribani kilomita tatu na upana  wa mita 200 limepungua ukubwa wake kwa karibu nusu ya uwezo wa awali kwa sababu za kujaa tope, matumizi mabaya, kukosa ukarabati na usimamizi.

Aidha limeota magugu maji ambayo inaua kizazi cha samaki na  kuvuruga  uvuvi.

DSC_0072

Mkuu wa wilaya ya Same, Herman Kapufi akisisitiza jambo kwenye kongamano hilo lililowakutanisha madiwani wa kata za halmshauri ya wilaya ya Same na wataalam kutoka UNCDF kujadili pamoja kabla ya utekelezaji.

DSC_0082

Pichani juu na chini ni washiriki wa kongamano hilo la siku moja ambao ni madiwani wa kata za Same, mainjinia  na wakandarasi kutoka halmashauri ya wilaya ya Same pamoja na wataalam kutoka UNDCF.

DSC_0028

DSC_0096

Washiriki wakitamaza video ya bwawa la Kalemawe lililopo wilayani Same mkoani Kilimanjaro kujionea hali halisi ya bwawa hilo linalohitaji ukarabati.

20140626_124641

Pichani juu na chini ni muonekano wa bwawa la Kalemawe lililopo wilayani Same mkoani Kilimanjaro wakati UNCDF walipotembelea eneo hilo.

20140626_124736

PICHA NA STORI: ZAINUL MZIGE

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO