Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

SERIKALI YA JAMHURI YA KOREA YAKUBALI KUTOA FEDHA KWA AJILI YA UJENZI WA DARAJA JIPYA LA SALENDER JIJINI DAR

Serikali ya Jamhuri ya Korea ya Kusini hatimae imekubali kutoa fedha kwa ajili ya kuanza Ujenzi wa Daraja jipya la kisasa la Salender. Daraja hili litakuwa mbadala wa daraja la Zamani la Salender.


Serikali hiyo imekubali kutoa mkopo wa fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Daraja hilo jipya na la kisasa kabisa litakalopita baharini pembezoni mwa Daraja la zamani la Salender kuanzia Coco Beachi (Oysterbay) kwenda Hospitali ya Aga Khan (Maeneo ya Ocean Road/ Baraka Obama Road).

KWA HABARI KAMILI
KON’GOLI HAPA

 

Muonekano wa Daraja jipya la Salenda litaakalopita baharini kuanzia Coco Beachi (Oysterbay) kwenda Hospitali ya Aga Khan (Maeneo ya Ocean Road/ Baraka Obama Road). Daraja hilo pamoja na barabara zake, litakuwa na urefu wa kilomita 7.2 na uwezo wa kupitisha magari zaidi ya 61,000 kwa siku huku likiwa na njia nne za magari pamoja service road njia za waenda kwa miguu kila upande

Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kulia akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini, Chung Il wapili kushoto kuhusiana na mambo mbalimbali kuhusu sekta ya Ujenzi pamoja na mchakato wa Ujenzi wa Daraja jipya la Salenda litakalopita baharini. Wa kwanza kushoto ni mke wa Balozi huyo.

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO