Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MO DEWJI ANYAKUA TUZO YA MWAKA YA MFANYABIASHARA ANAYESAIDIA ZAIDI JAMII

IMG_9463

Mkurugenzi Mtendaji wa CNBC Africa, Roberta Naicker akimkabidhi tuzo ya '2015 Philanthropist of the year-East Africa' Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji katika sherehe zilizofanyika hoteli ya DusitD2 jijini Nairobi.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog).

IMG_9492

Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji akizungumza kwenye hafla ya tuzo za All Africa Business Leaders Awards 2015 (AABLA). Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa CNBC Africa, Roberta Naicker.

IMG_9595

Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji akipozi katika picha ya kumbukumbu na Mkurugenzi Mtendaji wa CNBC Africa, Roberta Naicker.

IMG_9627

Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji akiwa ameshikilia tuzo yake.

IMG_9608

Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji akibadilishana mawazo na baadhi ya wafanyabiashara wakubwa jijini Nairobi ambapo pia walimpongeza.

IMG_9587

Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji katika picha ya kumbukumbu na mmoja wa wageni waalikwa kwenye hafla ya tuzo za All Africa Business Leaders Awards 2015 zilizofanyika kwenye hoteli ya Dusit D2 jijini Nairobi.

IMG_9655

Mohammed Dewji, CEO of MeTL Group....2015 Philanthropist of the Year-East Africa.

Na Mwandishi Wetu

BILIONEA anayemiliki kampuni kubwa ya Mohammed Enterprises nchini (MeTL), Mohammed Dewji `Mo’ ameshinda Tuzo ya Mfanyabiashara wa Mwaka anayejitoa zaidi kuisaidia jamii kunufaika kutokana na biashara zake, akiwa mshindi wa Afrika, Kanda ya nchi za Afrika Mashariki katika tuzo zilizofanyika juzi jijini Nairobi, Kenya.

Katika tuzo hiyo ya heshima kwa wafanyabiashara Afrika inayoratibiwa na Kituo cha Biashara cha Televisheni ya CNBC Afrika, Dewji alishindanishwa na mabilionea raia wa Kenya, Ashok Shah wa kampuni ya Apollo Investment Limited na Damaris Too-Kimondo anayemilikia kampuni ya Shrand Promotions.

Katika sherehe hizo zilizofana, Dewji alikabidhiwa tuzo yake na Mkurugenzi Mtendaji wa CNBC Africa, Roberta Naicker.

Ushindi wake umechangiwa kwa kiasi kikubwa na kitendo cha Dewji ambaye pia ni mwanasiasa aliyekuwa mbunge wa Singida Mjini kwa miaka kumi, kujihusisha na misaada yenye lengo la kupambana na umasikini kupitia sekta mbalimbali kama elimu, maji, watu wenye ulemavu na pia uwezeshaji kiuchumi, matukio ambayo yamelenga na kubadili hali ya watu maskini zaidi katika jamii.

Washindi hao wa Kanda ya Afrika Mashariki watashindanishwa na washindi wengine kutoka Kanda ya Kusini mwa Afrika na Afrika Magharibi Novemba 13, mwaka huu huko Sandton, Johannesburg nchini Afrika Kusini ili kupata mshindi wa jumla wa bara la Afrika.

Akizungumza mara baada ya kutunukiwa tuzo yake hiyo yenye heshima kubwa, aliwashukuru waandaaji, jarida la Forbes na majaji kwa kumuona anastahili kwa tuzo hiyo ya kipekee.

Alisema, kwake ni faraja kubwa kupata heshima huyo na amekuwa na ndoto za kusaidia watu wa Tanzania kukabiliana na changamoto wa kasi ya maendeleo barani Afrika na kwamba ili kuendana na kasi hiyo, miongoni mwa juhudi zinazotakiwa ni kuwawezesha kupata elimu bora, hasa wa maeneo ya vijijini.

“Ninaamini tukiunganisha nguvu, nchi za Afrika zina nafasi kubwa ya kuwa na wataalamu wake watakaosaidia kusukuma gurudumu la kiuchumi Afrika na hivyo kuboresha hali za maisha za watu wa bara hili,” alisema bilionea huyo kijana aliyeanzishwa taasisi yake ya Mo Dewji Foundation kwa lengo la kuisaidia jamii.

Alisema kwamba hilo ni tukio kubwa sana kwake na kumnukuu Maya Angelou, akisema: “Ukisoma, fundisha. Ukipata, toa.” Aliongeza kuwa, kwa kuwa amebarikiwa na Mungu kupata vyote, anakusudia kuendelea kuuelimisha umma juu ya kufanya mapinduzi ya kielimu, afya, na maeneo mengine ya ustawi wa jamii, huku akiahidi kusaidia kwa kila atakachojaliwa.

Dewji mwenye umri wa 40 ambaye kwa sasa ndiye bilionea kijana zaidi Afrika kwa vijana wasiozidi umri huo, akiwa pia miongoni mwa mabilionea 55 wanaoongoza kwa utajiri Afrika, anaongoza kampuni yenye makampuni yaliyojikita katika sekta za kilimo, fedha, uzalishaji, usambazaji wa bidhaa na kadhalika, huku akitajwa kuajiri zaidi ya watu 20,000.

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO