Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MGOMBEA UBUNGE CHADEMA JIMBO LA HANANG, DERICK MAGOMA ADAI HAWANA IMANI NA MSIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO HUMO

Mgombea Ubunge Jimbo la Hanang Derick Magoma akizungumza na waandishi wa

Habari (hawapo pichani) juu ya kutokua na imani na Msimamizi wa Uchaguzi wa

Jimbo hilo ambaye ni Mkurugenzi wa Wilaya ya Hanang Felix Mabula madai

ambayo wamewasilisha kwa tume ya uchaguzi iteue Msimamizi ili kufanikisha

uchaguzi huru na wa haki.Kushoto ni Mwenyekiti wa Chadema Hanan`g  Isack

Joseph  na kulia ni Mgombea udiwani kata ya Endasiwold John Farayo habari 
___________________________ 

Wagombea wa Nafasi za Ubunge na Udiwani katika Wilaya ya Hanang iliyoko

mkoa wa Manyara wamedai kutokua na imani na Mkurugenzi wa Halmashauri ya

Hanang , Felix Mabula ambaye ni Msimamizi mkuu wa uchaguzi katika jimbo

hilo kwa madai kuwa Mkurugenzi huyo alikumbwa na tuhuma nyingi za matumizi

mabaya ya fedha kwenye miradi ya maji na kuboresha miundombinu ya shule za

msingi tuhuma ambazo ziliibuliwa na madiwani wa CHADEMA  ambao ni wagombea

kwa sasa jambo linalowapa wasiwasi kuwa haki haitatendeka katika uchaguzi.


Mgombea Ubunge katika jimbo la Hanang Derick Magoma alisema hayo wakati

akizungumza na Waandishi wa Habari ,amesema kuwa tayari wameandikia barua

tume ya Uchaguzi yenye kumbukumbu namba CDM/HAN/UT/2/239  juu ya kutokua na

imani na msimamizi wa Uchaguzi wa jimbo hilo barua waliyoiwasilisha

septemba 2 mwaka huu wakiitaka tume iteue Msimamizi mwingine.


Magoma alisema kuwa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha zilijadiliwa katika

Baraza la Madiwani zikiongozwa na madiwani wa CHADEMA ambao ni Ndugu Peter

Lori Diwani wa Kata ya Katesh,John Farayo Diwani kata ya Endasiwold ,Masala

Bajuta wa kata ya Gisambalang na wengine wengi.


“Madiwani hao waliomtuhumu Mabula  ndio wagombea    na hao hao Mabula

atasimamia uchaguzi wao ,tunaona kabisa kuwa haki haiwezi kutendeka ,na

hata kama ikitendeka hatutaamini kama imetendeka” Alisema Magoma


Mgombea huyo alisema kuwa Mabula anakabiliwa na tuhuma za kutumia vibaya

shilingi bilioni 1 na milioni 100 ambazo zimepotea na zingetumika kujenga

vituo vya afya ,kuleta madawa na kusambaza huduma ya maji safi ambayo ni

changamoto kubwa kwa jimbo hilo.


Mgombea udiwani kata ya Endasiwold John Farayo alisema kuwa wao kama

wagombea hawana imani na Mkurugenzi huyo hivyo wameitaka tume ya uchaguzi

ichukue hatua za haraka kumteua msimamizi mwingine wa uchaguzi ili uchaguzi

uwe huru na wa haki.


Mwenyekiti wa Chadema Hanan`g  Isack Joseph alisema kuwa chama hicho

kimesimamisha wagombea  udiwani 31 kati ya kata 33 na kufafanua kuwa

kutokana na rekodi ya Mkurugenzi huyo wanahitaji msimamizi mwingine wa

uchaguzi ambaye watakua na imani naye.

Picha/Stori: Woinde Shizza

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO