Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MAGUFULI AHIDI KUFUFUA VIWANDA MKOANI TANGA,KUONGEZA AJIRA KWA VIJANA

 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi (CCM),Dkt John Pombe Magufuli akifafanua jambo mbele ya maelfu ya wakazi wa jiji la Tanga waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni,uliofanyika katika viwanja vya Tangamano jioni ya leo mjini Tanga. 
  Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa mji wa Tanga kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya angamano,jioni ya leo ambapo aliahidi kuboresha Bandari ya Tanga, kujenga Viwanda vya matunda na samaki ili kuweza kupunguza tatizo kubwa la ajira kwa vijana.
 Naibu Waziri wa Sheria na Katiba,ambaye pia ni mgombea Ubunge viti maalum upande wa akina Mama mkoa wa Tanga (UWT),Mh Ummy Mwalimu akimuombea Kura za kutosha mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli ili aweze kuibuka mshindi na kuiongoza Tanzania katika awamu ya tano.
 Wakazi wa mji wa Tanga waliofika kwenye mkutano huo wakishangilia jambo. 
 Nyomi la watu . 
 Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli akisalimiana na  Naibu Waziri wa Fedha na mgombea ubunge wa Jimbo la Iramba  Magharibi Mheshimiwa Mwigulu Nchemba
  Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia  ambaye pia ni mgombea Ubunge wa Jimbo la Bumbuli Mhe. January Makamba akihutubia wakazi wa mji wa Tanga kwenye mkutano wa kampeni za CCM.
 Sehemu ya umati wa wakazi wa mji wa Tanga na vitongoji vyake wakiwa wamefurika kwenye viwanja vya Tangamano kwenye mkutano wa kampeni za CCM,ambapo Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli aliwahutubia wananchi hao.

 Dkt Magufuli akisisitiza jambo mbele ya maelfu ya wananchi (hawapo pichani) jioni ya leo kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika uwanja wa Tangamano.
  Naibu Waziri wa Fedha na mgombea ubunge wa Jimbo la Iramba  Magharibi Mheshimiwa Mwigulu Nchemba akihutubia wakazi wa Tanga mjini kwenye mkutano uliofanyika kwenye uwanja wa Tangamano. 
  Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia  ambaye pia ni mgombea Ubunge wa Jimbo la Bumbuli Mhe. January Makamba na Naibu Waziri wa Fedha na mgombea ubunge wa Jimbo la Iramba  Magharibi Mheshimiwa Mwigulu Nchemba wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye mkutano wa kampeni jioni ya leo katika uwanja wa Tangamano,ambapo Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli alihutubia na Kumwaga sera zake kwa wananchi,ikiweno na kuomba ridhaa ya kuwaongoza katika miaka mitano ijayo.
 Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM Mzee Yusuph Makamba akihutubia wakazi wa Tanga mjini kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika ndani ya viwanja vya Tangamano.
 Maelfu ya Wananchi wakimsikiliza Dkt Magufuli alipokuwa akimwaga sera zake na kuwaomba wananchi hao wajitokeze kwa wingi Oktoba 25 na kumpigia kura ya ndio ili aibuke mshindi na kupewa ridhaa ya kuiongoza Tanzania katika awamu ya tano.
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwaaga wananchi wa mji wa Tanga waliofika kwenye mkutano hadhara wa kampeni,uliofanyika jioni ya leo katika viwanja vya Tangamano mjini humo na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa watu.

PICHA NA MICHUZI JR-TANGA
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO