Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

VYUO VIKUU NCHINI KUNOANA KATIKA KONGAMANO LA ELIMU YA JUU 2015 JIJINI ARUSHA

 

  

Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), Profesa Yunus Mgaya akizungumza na waandishi habari leo kuhusu kongamano la saba la elimu ya juu 2015 linalotarajiwa kufanyika jijini Arusha kuanzia Oktoba 1-2, 2015. Pembeni ni Thea Mtau (kulia) na Cosmas Mwasoibya ambao ni wajumbe wa Kamati ya Maandalizi.

Waandsihi wakimsikiliza   Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), Profesa Yunus Mgaya katika mkutano na waandsihi wa habari uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii/Picha na Cathbert Kajuna.

WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kushirikiana na Tume ya Vyuo Vikuu nchini ,Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) pamoja na Kamati ya Wakuu wa vuo Vikuu nchini (CVCPT) imeandaa kongamano la saba la elimu.

Akizungumza na waandishi habari leo jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), Profesa Yunus Mgaya amesema wazo la kuandaa makongamano ya elimu ya juu nchini ni kubadilishana uzoefu na maarifa miongoni mwa wadau elimu katika mstakabali wa taifa.

Amesema katika makongamano watajadili changamoto zinazokabili sekta ya elimu ya juu kutokana na kupanuka kwa sekta hiyo kwa kuwa uazishwaji wa vyuo vikuu binafsi na ongezeko la udahili vyuoni na mabadiliko mengine.

Profesa Mgaya amesema kongamano wanalotajia kulifanya ni la saba ambalo linatarajia kufanyika Oktoba 1 hadi 2 mwaka huu mkoani Arusha.

Amesema katika  kongamano hilo lina malengo ya kuangalia jukumu la Taasisi za Elimu juu nchini kusaidia maendeleo uwezo kwa kuzingatia elimu inayotolewa, Kubainisha fursa muhimu amabazo taasisi ya elimu zinaweza kutumia pamoja na mkakati wa itakayowezesha ushirikiano madhubuti baina ya sekta binafsi ya elimu ya juu,Viwanda na wadau wengine wa kuleta mabadilko katika sekta ya elimu nchini.

CREDIT: MICHUZI MEDIA

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO