Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MBIO ZA RIADHA ZA MOUNT MERU MARATHON KUTIMUA VUMBI OKTOBA 4, 2015 JIJINI ARUSHA

Na Woinde Shizza,Arusha

Baada ya kutokuwepo kwa mbio za riadha zijulikanazo kama mount meru Marathon kwa miaka 15 sasa ,hatimaye wadau wa mchezo wamjitokeza na kurudisha mbio hizo ambazo zinatarajiwa kufanyika  octoba 4 jijini Arusha.

Mbio hizo za km 21 zilifanyika mara ya mwisho mwaka 2000,ambapo hazikuendelea tena kutokana na kukosa wadhamini hali iliyopelekea kukosa hamasa kwa wanariadha  mabalimbali.

Katibu wa chama cha riadha mkoani hapa  Alfredo Shahanga alisema kwuwa mbio hizo ni za wazi na zitashirikisha wanariadha wanawake na wanaume mbalimbali  kutoka ndani na nje ya nchi  kwa wanariadha ambao watakuwa  tayari kuja kushiriki.


“Mashindano haya chimbuko lake ni mkoani hapa na mara ya mwisho kufanyika ilikuwa ni mwaka 2000 kipindi hicho yakiitwa ‘Mount meru International Marathon’ yalishindwa kuendelea kufanyika kutokana na  kuwa wale waandaaji wa miaka hiyo walifikia mahali  mahali wakasitisha kutokana na sababu za kifedha”alieleza Shahanga.

Mbio hizo zinaandaliwa na Mambo jambo digital centre kwa kushirikiana na chama cha riadha mkoani hapa  zitaanzia mnara wa saa  zitazunguka kuelekea barabra ya sokoine mpaka uwanja wa ndege baadae zitamalizikia uwanja wa mpira wa sheikh Amri Abeid.

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO