Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

WARSHA YA WADAU WA MRADI WA JALI ARDHI WAFANYIKA MONDULI



Inline images 3
Mkuu wa wilaya ya Monduli Idd Kimanta akiwa anazungumza na wadau mbalimbali waliohudhuria katika Warsha ya wadau wa Jali Ardhi ya siku mbili iliyoandaliwa na Chuo kikuu cha Nelson Mandela Arusha kwa kushirikiana na Shirika la maendeleo kutoka nchini Uingereza.Picha na
Carey Marks
Inline images 4
Pichani ni mkuu wa wilaya ya Monduli Idd Kimanta akiwa anasisitiza jambo aliyepo katikati ni  Dkt.Kelvin Mtei kutoka Chuo cha Sayansi cha Nelson Mandela,akifuatiwa na aliyepo kulia kwake ni ndugu Charles Bonaventure kutoka Taasisi ya shirika lisilo la kiserikali linalohusika na uhakikawa chakula na kustawisha mazin wa mazao na chakula (ECHO)Picha na Carey Marks

Inline images 2
Wadau waliohudhuria warsha ya jali Ardhi wakiwa wanamsikiliza Profesa Profesa wa Sayansi za kilimo kutoka Taasisiya Sayansi na Teknolojia cha  Nelson Mandela Arusha,Patrick Ndakidemi.Picha na Carey Marks
Inline images 1
Picha ya pamoja ya wadau wa Warsha ya wadau wa Jali Ardhi.Picha na Carey Marks



Na.Vero Ignatus,Monduli

Chuo kikuu cha  Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela Arusha kwa kusirikiana na Shirika la maendeleo kutoka nchini Uingereza (DfID)  wameandaa warsha ikiwa na lengo la kujadili matukio ya kitafiti ya sababu za mmomonyoko wa ardhi uliochangiwa na matukio yaliyowahi kutokea hapo zamani,sasa na changamoto zijazo katika wilaya ya Monduli. 


 
Akizungumza katika ufunguzi wa warsha hiyo mkuu wa wilaya ya monduli Idd Kimanta ambaye alimuwakilisha mkuu wa mkoa wa Arusha amesema kuwa sababu kubwa ambazo zinasababisha mmomonyoko wa ardhi ni pamoja na mifugo mingi zaidi ya maeneo ya malisho,kilimo cha mfululizo,kilimo katika maeneo yanayomomonyoka kwa urahisi ,ukataji wa misitu,tabia za jamii zinazohama,mifumo ya umiliki ardhi ,kuongezeka kwa kubwa idadi ya watu ,mabadiliko ya tabia nchi na mahitakji ya nishati
 .
Aidha amesema kuwa zipo hatua ambazo zinaweza kuchukuliwa katika kuzuia mmomonyoko wa ardhi kwa kuhifadhi uoto wa asili,kupunguza kasi ya maji kwa kuweka matuta,kutandaza majani katika ardhi haswa kwa kuotesha mimea jamii ya mikunde pamoja na kuhifadhi uoto wa asili.

Akizungumzia utafiti huo Profesa wa Sayansi za kilimo kutoka Taasisiya Sayansi na Teknolojia cha  Nelson Mandela Arusha,Patrick Ndakidemi amesema kuwa utafiti huo ulianza rasmi novemba 2016 ukiwa na lengo la kupata majibu ya kitaalamu yanayosababisha mmomonyoko wa ardhi ambapo utafiti huo unatarajiwa kukamilika julai 2017


Nae mtafiti kutoka Chuo cha Sayansi cha Nelson Mandela Dkt.Kelvin Mtei amesema kuwa katika wilaya ya monduli mmomonyoko husababishwa na  maji kutiririka juu ya ardhi na huchukua virutubisho kwenye udongo ,kukoseka na kwa uoto,mafuriko pale maji yanaposhindwa kupenya kwenye udongo nakusababisha uharibifu.

Dkt.Kelvin amesema kuwa  mmomonyoko wa ardhi umeanza kuongezeka miaka 20 iliyopita,ambapo maporomoko yameongezeka zaidi miaka 10 iliyopita, mmomonyoko huo unapeleka tope ziwani ambapo amesema utafiti huo walianza kwa kupima upenyaji wa maji kwenye ardhi,kulinganisha umomonyokaji,kupima kiasi cha mmomonyoko,upimaji kupitia picha za setilaiti na wakafanya uchunguzi wa tope kwenye mahabara .


Sambamba na hayo baadhi ya washiriki wa warsha hiyo ambao hawakutaka kutaja majina yao wameiomba serikali ipitishe sheria itakayombana mfugaji asiwe na zaidi ya ng'ombe watano ambao ataweza kuwakuwahudumia na mfugaji huyo ataweza kutunza mazingira yake mwenyewe.


Warsha hiyo ya siku mbili imewashirikisha wadau mbalimbali wakiwemo watendaji wa vijiji vya Lendakenya ,Arkatan,watafiti kutoka chuo cha utafiti cha Seliani Arusha,Washiriki wa mashirika yasiyo ya kiserikali,ECHO,UJAMAA,TANAPA na MVIWATA,Wakulima na wafugaji kutokaa Monduli,Watafiti kutoka vyuo vikuu vya Plymouth,Exeter,na Schumacker ;Uingereza,Taasisi ya Sayansi na Tekinolojia ya Nelson Mandela.



Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO