Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Rais wa TLS Wakili Lissu Ahofia Taasisi Hiyo Kufutwa, Aita Mkutano wa Dharura wa Wanasheria


Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kimeitisha mkutano wa dharula wa wanasheria nchi nzima kwa ajili ya kujadili mapendekezo na kutoa msimamo wao dhidi ya Serikali ya kuanzisha Bodi ya Usajili ya Mawakili.

Akizumza jana  kwenye mkutano huo Rais wa TLS, Tundu Lissu alisema mapendekezo yaliyotolewa ni hatari kwa uhuru wa TLS na kada ya sheria kwa ujumla iwapo siasa itaingia kwenye kazi zao za sheria.

Alisema bodi hiyo ikianzishwa itakuwa chini ya waziri wa sheria na katiba na ndiyo itakuwa na nguvu ya kusajili au kuwafuta wanasheria kadri itakavyoona inafaa.

"Mabadiliko haya ni hatari sana kwa uhuru wa wanasheria nchini, tumekutana hapa kuelezana na kupokea maoni ya wanachama kisha tutaweka msimamo wetu baada ya baraza la TLS kukaa .
"Huo ni mkakati wa Serikali kuminya uhuru wa TLS ili kuwadhibiti wanasheria kuingia kwenye siasa, jambo ambalo  linatakiwa kupingwa na kila mtu kwa sababu matokeo yake ni mabaya"alisema Mh. Tundu Lissu.
 
Mbali na hayo Lissu aliwaasa wanasheria kuwa endapo watashindwa kusimamia taaluma yao vizuri na kuruhusu siasa ikaingia ndani yake basi haitokuwa na maana ya  kuwepo kwa chama hicho
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO