Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MAALIM SEIF AONGOZA HARAMBEE YA KUCHANGIA MADRASSA MUUMIN KIWALANI, UKAWA WAMSINDIKIZA


Katibu mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad akiongoza harambee ya uchangiaji wa Madrasa Kiwalani Temeke jijini Dar es Salaam ambapo aliwezesha kupatika kwafedha zaidi ya Milioni 7 kwa ajili ya ununuzi wa kiwanja kipya cha Madrasa hiyo

Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala , Omary Kumbilamoto akikabidhi mchango wake wa shilingi laki tatu katika harambee ya kuchangia Madrassa ya Muumini Islamiya iIliyopo kiwalani Dar es Salaam
Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita akikabidhi mchango wake kwa Katibu mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad kwa ajili ya Muumini islamiya.

Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita akizungumza wakati alipokuwakitoa ahadi yake ya Milioni moja kwa ajili ya Madrasa hiyo na aliweza kuwasilisha shilingi laki tano papo hapo na kuongeza ahadi ya bati 70 na mifuko 50 ya Saruji.
Diwani wa Kata Mianzini , Kassim Mshamu ambaye ndio mlezi wa Madrasa ya Muunin Islamiya akiwakaribisha wageni katika arambee yakuchangia madrasa
Sheikh Anuary Jongo akitoa Darasa juu ya waslamu na umuhimu wa kuchangia nyumba za ibada hili waweze kujenga ukaribu na Mungu hasa katika kumi hili la mwisho la mwezi mtukufu wa Ramadhani
Sehemu ya washiriki wa arambee hiyo wakipata futari iliyoandaliwa na Madrasa Muumin Islamiya
Katibu mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad akiteta na Mkurugenzi wa uchaguzi wa Chama Cha Wananchi CUF , Shaweji Mketo
Sehemu ya watoto wa Madrasa ya Muumini Islamiya wakipata futari mara baada ya kumalizika kwa harambee hiyo
Vijana wa Kiislamu wakitoa Nashid kwa ajili ya kuleta burudani kwa watu waliofika katika arambee hiyo
sehemu ya vijana wa Madrassa ya Muumin Islamiya wakinyosha mikono wakati wa utambulisho

PICHA NA MICHUZI BLOG
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO