Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Naibu Meya Jiji la Arusha Aachiwa na Polisi; Kuripoti tena Kituoni Jumatano Juni 28 mwaka huu



Naibu Meya wa  Halmashauri ya Jiji la Arusha Mh Viola Likindikoki (watatu kutoka kulia) akiwa na viongozi wa BAWACHA Arusha  pamoja na madiwani wenzake waliokuwa wamekamatwa na kushikiliwa na Polisi tangu saa tisa alasiri jana mpaka usiku wa kuamkia leo majira ya saa sita walipoachiwa kwa sharti la kuripoti tena kituo kikuu cha Polisi Arusha leo asubuhi. Viongozi hao waliripoti hiyo asubuhi leo na kuelekezwa kurudi tena siku ya Jumatano Juni 28 mwaka huu.

Taarifa ambazo blogu hii imezipata zinaeleza kuwa katika kukamatwa kwao na kupelekwa kitengo cha makosa ya mitandao, kuna simu ya Naibu Meya huyo Polisi wanaitafuta, ambapo pia na mwenye nayo nae anaitafuta kwani anadai alinyang'anywa mkoba wake uliokua na vitu vyake vyote. 

Dodoso zetu zinaonesha kuna malalamiko kutoka kwa Mkurugenzi wa Jiji  kwenda kwa Jeshi la Polisi kuhusiana na taarifa fulani ambazo zinadaiwa kuwa za siri na mkurugenzi kuwahisi viongozi haohuenda ndio waliovujisha. 



Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO