Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Kisa cha Diwwani wa CHADEMA Arusha Aliyejiuzulu!


DIWANI wa Kata ya Murriet mkoani Arusha kupitia Chama Cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA) Credo Kifukwe ajiuzulu nafasi yake.

Kifukwe amesema kuwa ameamua kujiuzulu nafasi yake ili aweze kupata muda na nafasi ya kuitumikia wananchi na familia yake na bila kuweka itikadi mbele.

"Ninajiuzulu nafasi yangu ili niweze kumuunga mkono Rais Magufuli katika utendaji wake, dhamira inanisuta kuwa katika kundi linalopinga kila kitu mimi binafsi nipo tayari kushirikiana bega kwa bega" alisema Kifukwe.

Wakati huo huo, Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Arusha Amani Golugwa akalizungumzia tukio hilo na kueleza kwamba 


"Wanaotaka kuondoka waondoke sasa, kazi tuliyo nayo ni kubwa mbele yetu. Kamwe hatutahesabu hasara yoyote kuondoka. Kazi iliyopo mbele yetu ni kubwa na yenye kuhitaji kujitoa kwa dhati. WanaCHADEMA msisikitike, wamechelewa kuondoka na msione kuwa wanatushtukiza, hapana wao ndio wamekaa kwa mateso sana na sasa hawana budi kuondoka maana hawakuwa Wa kwetu. 

 Yai likishakuwa viza halina thamani tena ya kukaa kwenye trei LA mayai mazuri". Wataondoka kadhaa, tusipaniki tuwaache waondoke, tulijua baadhi yao wataondoka na tunajua baadhi yao wapo njiani kuondoka, tuwaache waondoke kwa kujichinja wenyewe. 

Kazi iliyopo mbele yetu ni kubwa na inahitaji waliojitoa hasa na wenye mapenzi mema na nchi hii na sio unafiki. Hila yao kwa kupindi walicho kaa nasi na dhambi yao ya maneno ya uongo wakati wa kuondoka kwao watailipa tu"

Blogu hii ilimtafuta Mwenyekiti wa CHADEMA WIlaya ya Arusha Mjini Derick Magoma ambaye alieleza kwa kifupi kuwa ndio  anaingia nchini toka safarini na hajapata taarifa rasmi ya maandishi kama taratibu zilivyo kuthibitisha kujiuzulu kwa Diwani huyo ingawa alisisitiza kuwa kulikuwa na masuala ya kindidhamu dhidi yake yalikuwa yanaendelea ndani ya chama. 
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO