Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Meya wa Jiji la Arusha Kalisi Lazaro Ampa Siku Saba RC Gambo Amuombe Radhi Kwa Kumuweka Kizuizini Bila Hatia Vinginevyo Atamburuza Kortini

Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha, Mh Kalisti Bukhay Lazaro

MKUU wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo ametakiwa kujitathimini iwapo anastahili kuendelea kuwa mtumishi wa umma katika nafasi aliyonayo baada ya kutiwa hatiani na mahakama kuu mkoa wa Tanga na kutakiwa kulipa kiasi cha shilingi milioni 20 kwa kosa la kumdhalilisha  mtumishi mwenzake kwa matusi.

Kesi hiyo namba 4 ya mwaka 2015,Gambo alikata rufaa mahakama kuu ,kupinga hukumu iliyotolewa na mahakama za chini,katika kesi ya madai iliyofunguliwa na mlalamikaji ,Najum  Tekka ambaye ni mwanasheria wa halmashauri wilaya ya Korogwe aliyekuwa akimlalamikia Gambo kumtolea lugha ya kumdhalilisha  kuwa anadigrii ya nguo ya ndani(chupi).

Kwa mujibu wa  hukumu hiyo nakala tunayo, iliyotolewa, Septemba 9 mwaka 2016 na jaji  Amour Khamis wa mahakama kuu,mkoani humo,meya wa jiji la Arusha, Kalisti Lazaro  alisema kuwa Gambo amekaidi kulipa kiasi hicho cha fedha kilichoamuriwa na mahakama.

Aidha meya alitoa siku saba kwa kumtaka  gambo kuomba radhi kwa wanawake wote Tanzania kwa kosa la kumdhalilisha mwenzao na kwamba kinyume na hapo atahamasisha wanawake wote Arusha waandamane kupinga kitendo hicho .

Akizungumzia mwenendo wa utendaji wa Gambo katika mkoa wa Arusha,Meya wa jiji la Arusha jana, Mh Kalist Lazaro alimshauri kiongozi huyo kuangalia uwezekano wa kujiweka pembeni na madaraka aliyonayo kwa kukosa sifa na kimaadili ya kiutumishi baada ya kuwepo kwa msuguano usiokoma na baadhi ya watumishi wenzake.

Aidha alisema tangu kutolewa kwa hukumu hiyo ,Gambo amekuwa msiri na amemficha rais John Magufuli kumweleza ukweli wa mwenendo wa kesi hiyo hadi alipoteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Arusha,jambo ambalo ni kimyume cha kanuni za utumishi wa umma.

Meya amemtaka kutekeleza mambo matano ikiwa ni pamoja na kulipa fidia na gharama zote zilizoamuriwa na mahakama ,aombe radhi kwa mwanamke aliyemkashifu  kuwa anadigrii ya chupi,pia awaombe radhi wanawake wote Tanzania.

Pia alimtaka atafakari upya kiapo chake mbele ya rais  kama bado anastahili kuwa kiongozi wa umma hasa ukizingatia kuwa alimficha rais kwa kiapo alichoapa wakati  anafahamu wazi kuwa alishahukumiwa kwa kosa la uadilifu.

‘’Iwapo kama Gambo hata tekeleza mambo yote matano niliyotaka ayafanye ,nimejipanga mimi na wanasheria wangu tutamfikisha mahakamani kuiomba mahakama ikamate mali zake ambazo tunazijuia ikiwemo nyumba yake iliyopo Muriet jijini Arusha’’alisema meya Lazaro.
Image result for mrisho gambo
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mh Mrisho Mashaka Gambo
Naye wakili George Magoti aliyekuwa akimtetea mlalamikaji katika kesi hiyo,alisema kuwa anajipanga kukaza hukumu iliyotolewa na mahakama hiyo kwani licha ya mahakama hiyo kumtia hatiani kwa kumtaka kulipa kiasi hicho cha fedha ,hadi hivi sasa hajatekeleza amri hiyo.
Alisema kuwa mahakama ilimwamuru kulipa kiasi cha shilingi milioni 20 kama fidia kwa mlalamikaji,shilingi milioni 5 gharama za uendeshaji wa kesi na asilimia 7 ya riba tangu kuanza kwa kesi mwaka 2015 na kwamba kiasi hicho cha fedha kitaongezeka kutokana na muda ulioamuriwa kupita.
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO