Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

KILI STARS, ZANZIBAR HEROES KUUMANA KUWANIA NAFASI YA TATU CHALENJI CUP; KENYA NA UGANDA KUKIPIGA FAINALI

TIMU ya Taifa ya Tanzania Bara 'Kilimanjaro Stars' na ile ya Zanzibar 'Zanzibar Heroes' sasa zitakutana katika mechi ya kusaka mshindi tatu wa michuano ya kombe la Chalenji inayofikia tamati kesho nchini Uganda kwa kuzikutanisha katika hauta ya fainali Kenya na Uganda ambae ni mwenyeji wa michuano hiyo na bingwa mtetezi.

Timu hizo zitakutana katika mchezo huo leo baada ya jana kufungwa katika michezo yao ya nusu fainali ambapo Zanzibar Heroes ilitolewa kwa matuta na Kenya baada dakika 120 kumalizika kwa sare ya mabao 2-2, huku Kilimanjaro Stars ikifungwa na Uganda mabao 3-0 yaliyopachikwa wavuni na washambuliaji Emmanuel Okwi na Robert Snetongo.

Wachezaji wa Bara wakijadiliana baada ya kufungwa na Uganda katika mchezo wa Nusu Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge usiku wa leo kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole mjini Kampala, Uganda. Uganda walishinda 3-0 na kutinga fainali, ambako watamenyana na Kenya kesho  

SURA ZA HUZUNI; Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe kulia akifuatilia mchezo kati ya Bara na Uganda. Kushoto wake ni Waandishi wa Habari wa Tanzania, Somoe Ng'itu juu na Zaituni Kibwana pembe ni kabisa Z.H.

Cheki ulinzi huo langoni mwa Uganda, Ngassa na Bocco peke yao wangefanya nini

Amri Kiemba anakokota ngoma

John Bocco akiwa amezibiwa njia

John Bocco leo aliwekewa ulinzi mkali, kama unavyona hapa

Mrisho Ngassa akidhibitiwa na beki wa Uganda

Mwinyi Kazimoto akijaribu kufumua shuti mbele ya beki wa Uganda

Kipa kadaka, Ngassa na Bocco leo hoi

Kocha wa Stars, Kim Poulsen baada ya mechi

Kapteni Kaseja haamini macho yake

Emmanuel Okwi akifuatilia mchezo benchi baada ya kuumia na kutoka

Bocco mawindoni, lakini ulinzi wa kutosha ulimynima mabao leo

MATUKIO YA MAPAMBANO BAINA YA KENYA NA ZANZIBAR HEROES

Beki wa Zanzibar, Aggrey Morris akishangilia baada ya kuifungia timu yake bao la pili kwa penalti, Uwanja wa Mandela, Namboole katika Nusu Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge usiku wa leo. Zanzibar ilifungwa kwa penalti 4-2 na sasa itamenyana na Bara katika mchezo wa kusaka mshindi wa tatu Jumamosi.

Khamis Mcha 'Vialli' akishangilia baada ya kuifungia Zanzibar bao la kwanza

Adeyom Saleh Ahmed akimtoka beki wa Kenya, Joackins Atudo

Nadir Cannavaro ameruka na kipa wa Kenya

Mcha anapasua ukuta wa Kenya

Mcha Vialli kamlamba mtu chenga, kamuacha chini anaambaa

Suleiman Kassim 'Selembe' akipasua katikati ya msitu wa wachezaji wa Kenya

Kocha wa makipa wa Zanzibar, Farouk Ramadhan akimpa maelekezo kabla ya mechi kipa Mwadini Ally

Kikosi cha Zanzibar

Kikosi cha Kenya

Wachezaji wa Zanzibar wakiwa wametahayari baada ya kufungwa bao la pili la kusawazisha

Mike Barasa wa pili kutoka kulia akishangilia bao lake la pili 

Zanzibar wakisujudu baada ya kufunga bao la kwanza

Kipa kaenda kulia, penalti ya Aggrey imetinga kushoto

Aggrey akiwaongoza wenzake baada ya kufunga bao la pili  

Jaku Juma akipambana

Adeyom akimtoka beki wa Kenya

Adeyom anajaribu

Jaku Juma akipambana

Aggrey ameruka na mtu

PICHA ZOTE NA BIN ZUBEIRY BLOG

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO