Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MKOA WA ARUSHA KUKOMESHA MIGOGORO YA ARDHI

 Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo akizungumza kwenye kikao cha kutatua migogoro ya Ardhi mkoani humo

Serikali mkoani Arusha imejipanga ndani ya kipindi cha miaka miwili iwe imekomesha migogoro ya ardhi sanjari na mivutano ya mikapa ya kiutawala kati ya wilaya moja na nyingine.

Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo alisema hayo kwenye kikao cha Ardhi,Kilimo,Mifugo na Mazingira kilichowaleta pamoja wakuu wa wilaya,Wakurugenzi na Wenyeviti wa halmashauri pamoja na maafisa wengine kujadili kwa kina mbinu za kumaliza migogoro hiyo.

Alisema baada ya uhakiki wa mipaka na ushauri kutolewa eneo husika lipo Kijiji au wilaya fulani kiongozi au mwananchi atakayehamasisha uvunjifu wa amani atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Awali Mpima Ardhi mkoa wa Arusha,Hamdoun Mansoor akiwasilisha taarifa ya sekta ya ardhi alisema imekua ikitoa maelekezo ya kusimamia uendelezaji katika maeneo ya vijiji na miji kwa kuzingatia sheri ya ardhi namba 5 ya ardhi ya vijiji na 4 ya mwaka 1999 kanuni na taratibu zake.

Alisema changamoto inayoikabili sekta yake ni ujenzi holela unaofanyika kwa kasi kubwa katika maeneo ambayo kisheria yametangazwa kuwa maeneo ya Mpango,ambayo hayaruhusiwi kuendelezwa bila kupata kibali kutoka kwenye mamlaka husika.

"Serikali hujikuta ikilipa fidia zisizo za lazima wakati wa kuendeleza miundombinu mbalimbali na inapotaka kupeleka huduma nyingine za kijamii kwenye maeneo hayo,"alisema Manssor.

Aliyataja maeneo ya umma yanayopaswa kuhifadhiwa kuwa ni pamoja hifadhi za misitu,maeneo oevu,maeneo yenye vilima,vyanzo vya maji,mabonde na kingo za mito.

Manssor alisema uwezo mdogo wa halmashauri kulipa fidia umefanya maendeo mengi kutopangwa na kupimwa na hivyo kuruhusu ukuaji wa kasi wa makazi holela katika maeneo mengi ya mkoa na wilaya zake.

Migogoro ya mipaka ngazi ya mkoa ni katika vijiji vya Ngabobo, Olkung'wado, Leguruki, Ngejusosia, Miririnyi wilayani Arumeru mkoa wa Arusha na Kijiji cha Lekirimuni wilaya ya Siha mkoa wa Kilimanjaro ambayo inasababishwa na tofauti ya matangazo ya serikali namba 135 la mwaka 1954.

CREDIT: VERO IGNATUS
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO