Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MAVAZI YA KHANGA YALIVYO SHINE KWENYE KHANGA PARTY ! 31/DECEMBER 2016



Usiku wa 31,December 2016 kuamkia mwaka mpya 2017 ndipo wanamitindo mbalimbali walikutana na kusherekea kwa pamoja Usiku wa Khanga yaani “Khanga Party”. Tukio hili kama lilivyo kuwa limetaarifiwa awali limefanyika Regency  Park Hotel.  Design mbalimbali za vazi la Khanga kutoka kwa wanamitindo zilioneshwa kwenye stage na kuzikonga mioyo za wadau pamoja na wahudhuriaji  usiku huo.

Kumbuka Party hii imeandaliwa na Mama wa Mtindo maarufu kama Asya Idarous Khamsin, mbali na burudani zilizo kuwepo pia kulikuwa na Red Carpet yenye sifa kubwa ya kuwakutanisha mastaa na mashabiki wao kuweza kupiga picha za pamoja kwa ajili ya kumbukumbu. Tunawatakia mwendelezo mwema na wenye baraka wadau na wanamitindo kutoka hapa Tanzania. (Cheers 2017)































Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO