Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MRISHO GAMBO AONYA WAWEKEZAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO NGORONGORO






Na Woinde Shizza,Arusha.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema kuwa serikali haitasita
kuwachukulia hatua wawekezaji wanaochochea migogoro katika wilaya ya
Ngorongoro na kusababisha uvunjifu wa amani hivyo kuchangia kuzorota kwa
shughuli za maendeleo.



Gambo ameyasema hayo katika ziara yake wilayani Ngorongoro inayolenga
kutatua migogoro wa pori tengefu lenye ukumbwa wa kilomita za mraba elfu
kumi na tano ambapo amekutana na wadau mbalimbali ikiwemo
wawekezaji,wafugaji pamoja na viongozi wa kiserikali.



Amesema kuwa serikali itawaondoa wawekezaji wanaochochea migogoro na
kuwagombanisha wananchi na serikali yao jambo ambalo halitafumbiwa
macho



Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro Rashid Taka amesema kuwa wako baadhi ya watu
wanaonufaika na migogoro hiyo hivyo kumalizika kwa migogoro hiyo kutaleta
manufaa kwa wananchi wengi kuliko kunufaisha kundi la watu
wachache



Kwa upande wake Naibu Waziri wa Wizara ya Mifugo,Kilimo na Uvuvi  ambaye
pia ni Mbunge wa Ngorongoro Wiliam Ole Nasha na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa
Arusha  Lekule Laizer wamesema kuwa utatuzi wa mgogoro huo utasaidia
kuepusha migongano ya kimaslahi na kuchochea shughuli za kimaendeleo badala
ya kutumia muda mwingi katika usuluhishi wa miigogoro hiyo




Mkuu wa Mkoa ameanza Ziara yake leo Wilayani Ngorongo na kesho atatembelea
katika vijiji mbalimbali ikiwa ni katika juhudi za kutatua mgogoro wa pori
tengefu katika wilaya hiyo.
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO