Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Salamu za MwakaMpya: Lowassa Aisihi Serikali Kuruhusu Kupingana Bila Kupigana, Kuheshimu Haki za Raia na Kuruhusu Demokrasia


Akitoa salamu zake za mwaka mpya kwa watanzania kupitia tangazo maalumu lililorushwa na Azam Tv mapema leo asubuhi, zaidi akizungumzia hali ya kisiasa nchini Lowassa amesema hakuna sababu ya kufanya siasa zakuumizana na kwamba watu wapingane kwa hoja na sera bila kupigana.

"Tupingane bila kupigana, turuhusu watuwafaye mijadala, turuhusu watu wafanye shughuli zao, turuhusu watu waoneshe mapenzi na watu wanaokubaliana nao bila kuwaambia kwasababu wewe ni CHADEMA basi hustahili kupata hiki,kufanya biashara hii. Hii nchihaiwezi kwenda kwa utaratibu huo. Tutoe nafasi ya kupingana bila kupigana, 

Nchi hii ni ya amani, tutasaidiana. Napendakumuhakikishia (Mh Rais) kwa nafasi yangu na chama changu, tutaheshimu sana demokrasia, malekezo na mamlakaya Rais lakini tunaomba pia nanyie mkaheshimu haki zetu na demokrasia yetu itekelezwe kwa haki na kwa uhakika" 



Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO