Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Madaktari Wa Kenya Wakataa Nyongeza Ya Mshahara

Madaktari wamekataa kiwango cha nyongeza ya mshahara walichoahidiwa na rais Uhuru Kenyatta ili kusitisha mgomo unaoendelea na badala yake kushinikiza utekelezaji kikamilifu wa makubaliano ya nyongeza ya mshahara ya mwaka-2013. Wakihutubia wanahabari jijini Nairobi hivi leo, maafisa wa baraza la ushauri la chama cha wahudumu wa afya  na wataalam wa meno walisema hawatakubali chochote ila kutekelezwa kwa makubaliano hayo ya mwaka 2013. Maafisa hao walisema makubaliano hayo yamejikita kwenye misingi ya sheria na serikali inafaa kuyatekeleza.
Wakati huo huo maafisa hao wanatarajiwa kuandaa mkutano na wizara ya fedha leo alasiri kujadili jinsi makubaliano hayo ya pamoja yatakavyotekelezwa. Nyongeza hiyo ambayo serikali imesema itagharimu walipa ushuru shilingi bilioni-4 kila mwaka ilipendekezwa mjini Mombasa siku ya Jumatano.
CHANZO: KBC TAIFA
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO