Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

James Ole Millya awasha moto wa M4C Simanjiro, apokewa kwa shangwe na kuchinjiwa ng'ombe saba

Juzi Jumamosi July 7, 2012, kamanda mpya wa CHADEMA ambae awali alikuwa Kiongoziwa Vijana (UVCCM) Arusha Ndg Kames Ole Millya aliambatana na makamanda wengine wa chama hicho kwenda Wilayani Simanjiro kusambaza ujumbe wa Vuguvugu la Mbadadiliko (M4C) kwa jamii ya maeneo hayo.

Mapokezi ya ujumbe wa Millya katika vijiji tofauti tofauti alivyotembelea yalikuwa ni ya furaha tupu ikiwa ni sambamba na kuchinja ng'ombe 7 na kuchoma nyama, kurukaruka na kuimba nyimbo za kitamaduni (Maasai culture)

Zifuatazo ni taswira za matukio tofauti ya ziara hiyo katika vijiji tofauti 

DSC03953

DSC04032

Picha juu, Millya (mwenye kombati) anazungumza na mzee wa kimila  mara baada ya kuwasili jijiji cha Olubousoieti. Picha chini ni baadhi ya wananchi waliojitokeza kumpokea kijijini hapo.

DSC03962 Zoezi la uchomaji nyama linaendelea..ililazimu kikosi kazi kuweka kambi mahali hapa kuweza kusubiria kitoweo hiki.

DSC03977 Wazungu nao wakaunga msafara kula nyama porini..

DSC04005 Nyama zilikuwa tamu sana. Mwingine mwenye kombati ni kamanda mwingine wa chama hicho toka Same, Ndg Christopher Mbajo

DSC04017 Hapa Millya akifafanua masuala mbalimbali kwa wananchi wa Simanjiro

DSC04022 Morani wa kimasai “wakipandisha mori” kitamaduni zaidi

DSC04064 Wakati wa kurudi, msafara wa Millya ulilazimishwa kusimama na kupewa supu kabala ya kurudi mjini

DSC04061 (PICHA ZOTE NA CHRIS MBAJO)

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO