Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

ROSE KAMILI AFUNGUA KESI KUZUIA DR SLAA ASIFUNGE NDOA KANISANI JUALI 21, MWENYEWE ASEMA HIZO NI SIASA

Tausi Ally
dk-slaa-safitop ROSE Kamili anayedai kuwa ni mke wa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, amefungua kesi Mahakama Kuu akiiomba isimamishe ndoa ya kiongozi huyo na mke mwingine inayotarajiwa kufungwa Julai 21, mwaka huu wilayani Karatu Mkoa wa Manyara. Dk Slaa anatarajia kufunga ndoa na mchumba wake wa siku nyingi, Josephine Mushumbusi.

Kamili ambaye ni Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), pia anaiomba Mahakama iamuru Dk Slaa amlipe Sh50 milioni za fidia aliyotumia kujihudumia pasipo matunzo ya mumewe huyo.

Mbunge huyo kupitia kwa Wakili wake, Joseph Thadayo, aniomba pia Mahakama iamuru Mushumbusi amlipe kiasi cha Sh500 milioni za fidia ya maumivu aliyoyapata kutokana na kitendo chake cha kuingilia ndoa yao.

Kesi hiyo namba nne ya mwaka 2012 iliyopangwa kusikilizwa na Jaji Lawrance Kaduli, inatarajiwa kutajwa kwa mara ya kwanza leo.
Katika hati hiyo ya madai, mbunge huyo anadai kuwa ndoa inayotarajiwa kufungwa kati ya Dk Slaa na Mushumbusi ni batili kwa sababu kuna ndoa nyingine halali na inayoendelea kuishi kati ya Slaa na Kamili iliyofungwa mwaka 1985.

Alidai baada ya kufugwa kwa ndoa hiyo, Juni 18, 1987 walifanikiwa kupata mtoto wa kike anayeitwa Emiliana Muchu na baadaye Septemba 23, 1988 walipata mtoto mwingine wa kiume, Linus Amsi.

Katika uhusiano wao, Dk Slaa akiwa ni Padri wa Kanisa Katoliki, alifanya taratibu zilizomwondosha katika nafasi hiyo na kuanza maisha ya familia.

Baada ya taratibu hizo, jamii ya Watanzania iliwatambua kama mume na mke na hata kumbukumbu za hati za kimataifa kama za kusafiria ziliwatambua kuwa wanandoa.

Kamili aliendelea kudai katika maelezo hayo kuwa yeye na Slaa waliishi maisha ya ndoa yenye amani yaliyowawezesha kupata mali kadhaa walizomiliki kwa pamoja ikiwemo nyumba iliyopo kwenye Kiwanja namba 609 Kitalu E iliyopo Sinza, Dar es Salaam, nyumba ya makazi iliyopo Kijiji cha Gongali huko Karatu na vifaa mbalimbali vya nyumbani.

Hati ya mashtaka imeendelea kudai kuwa uhusiano kati ya Slaa na Kamili, ulianza kuharibika mwaka 2009, baada ya mume huyo kuwa na uhusiano na mwanamke mwingine kinyume cha sheria… “Tangu mwaka huo 2009, Slaa akaitelekeza familia yake kwa kutoipatia huduma,” imeeleza hati hiyo.

Kamili anaiomba Mahakama iamuru kuwa yeye na Dk Slaa bado ni mke na mume na kwamba Mushumbusi aliingilia ndoa yao hivyo izuie ndoa inayotajiwa kufungwa Julai 21, mwaka huu huko Karatu, Manyara.

Kamili pia amewasilisha hati hiyo ya mashtaka kwa Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo akimweleza Askofu Mkuu huyo wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam kuwa moja ya Parokia za Dar es Salaam zina taarifa ya ndoa hiyo.

Nakala ya madai hayo pia imewasilishwa kwa Msajili wa Mahakama Kuu, Msajili wa Ndoa na kwa Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Mbulu.

Dk Slaa: Nimeyazoea
Alipotakiwa kuzungumzia kesi hiyo nje ya Mahakama, Dk Slaa alisema: “Hayo mambo nimeyazoea na kimsingi hayanipi shida yoyote.”

Alipoulizwa endapo anajipanga vipi kulipa fidia hiyo alijibu: “Kesi ni kesi hivyo siyo kila kinachoombwa kwenye kesi lazima kilipwe.”

Hata hivyo, Dk Slaa alisema asingependa kuzungumzia suala hilo kwa undani kwa kuwa liko kwa mawakili wake lakini akasema amebaini kuwa hizo ni hila na michezo michafu ya kisiasa.

“Kwanza siyo pingamizi moja tu, kuna pingamizi mbili mahakamani lakini kwa ufupi ifahamike kuwa hizo ni hila.”

CHANZO: MWANANCHI 12/07/2012

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO