Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MCHUNGAJI GWAJIMA AKANUSHA MTUHUMIWA WA KUMTEKA DR ULIMBOKA KUTUBU KANISANI KWAKE

IKIWA ni siku chache tu baada ya Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, kutangaza kupatikana na kumshikilia raia wa Kenya, Joshua Gitu Mhindi (31) kutokana na kuhusika kwake na tukio la kumteka na kumpiga Dkt. Steven Ulimboka, baada ya kuhojiwa na kukiri mwenyewe kuwa alihusika wakati akitubu katika Kanisa la Ufufuo na Uzima, Mchungaji Josephat Gwejima wa kanisa hilo lililopo Kawe jijini Dar es Salaam ameibuka na kukuruka futi mia kuhusu tukio hilo.

Mchungaji Gwejima, ametoa ufafanuzi huo jana mbele ya mamia ya waumini wake wakati wa ibada ya Jumapili asubuhi.

Mchungaji Gwejima, alisema kuwa jana na juzi, watu wengi wakuwa wakimpigia simu kutaka ufafanuzi juu ya jambo linalowahusu. Kwamba alipigiwa simu kutoka ndani na nje ya nchi, kwa hiyo na yeye (Gwejima) ameona alifafanue jambo hilo kabla ya ibada.

Bofya hapa kuungana na Blog ya Dj Sek kwa taarifa zaidi

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO