Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Taswira za Mkutano wa CHADEMA Wilayani Simanjiro jana; James Ole Millya, Lema wawa gumzo

Chama cha Demokrasia na Maendeleo kimeendelea na operesheni yake ya M4C kuzunguka maeneo mbalimbali ya nchi kujua mizizi ya matatizo mbalimbali yanayowakabili watanzania nchini kote, na kukiweka chama karibu zaidi na wananchi.

Safari hii ilikuwa ni zamu ya wakazi wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara kutembelewa na makamanda wa chama hicho hapo jana wakiongozwa na Mjumbe wa Kamati Kuu wa chama hicho Mh Godbless Lema.

Mh Lema aliambatana na viongozi na makamanda wengine wakiwemo wanachama wapya waliohamia chama hicho hivi karibuni kutokea CCM. Miongoni mwao ni pamoja na James Ole Millya, Ally Bananga na Alphonce Mawazo.

Jumla ya mikutano saba ilifanyika kwa siku ya jana, sita ikifanyika kwa kuruzu maeneo tofauti ya Simanjiro kwa kutumia helcopta na baadae kumalizia na mkutano mkubwa wa jioni katika uwanja wa shule ya msingi Mirerani iliyopo eneo la Mirerani. Lema, Mawazo na Millya ndio waliotumia chopa na wengine walitumia gari mpya za chama hicho kwa njia za barabara kutokea Arusha Mjini.

Picha zifuatazo zinaonesha taswira za matukio tofauti yaliyojiri…

SAM_2935 Wananchi waliohudhuria mkutano wa CHADEMA eneo la Mirerani jana

SAM_2755 Chopa inayotumiwa na CHADEMA ikijiandaa kupaa kutoka viwanja vya NMC Arusha kuelekea Simanjiro. Ndani yake wamo Mh Godbless Lema, Alphonce Mawazo na James Ole Millya.

SAM_2769 Mwendesha baiskeli huyu alikuwa kivutio kwa wananchi na bango lake alilofunga kwenye chombo chake cha usafiri na kuzunguka nalo mitaa ya Mirerani kabla ya ugeni wa kina Millya kuwasili mjini hapo majira ya jioni jana.

SAM_2773 Shughuli za uzinduzi wa matawi ya chama hicho katika viunga vya mji wa Mirerani. Hapa ni ofisi ya tawi la Ndesapesa. Anaezungumza na maikrofoni ni kamanda wa chama hicho na mtaalamu wa GPS

SAM_2779 Ally Bananga aliewahi kuwa mjumbe wa kmati kuu CCM akiwakilisha vijana Arusha kabla ya kuhamia chadema akiongea na wananchi wa Mirerani kupitia vipaza sauti vya gari la matangazo wakati msafara ukielekea uwanjani kuanza mkutano wa mwisho hapo jana.

SAM_2820  Ally Bananga akikaribishwa jukwani kuzungumza.

SAM_2858 Sehemu ya viongozi walioketi jukwaa kuu katika mkutano huo hapo jana

SAM_2861 James Ole Millya (alievaa rubega) akikaribishwa jukwaani na Ndg Alphonce Mawazo kuzungumza. Wote waliwahikuwa wananchama wa CCM kabla ya kuhamia CHADEMA mapema mwezi April.

SAM_2870 James Millya akizungumza na wananchi wa Mirerani

SAM_2900 Sehemu ya wananchi waliohdhuria wakifuatilia hotuba za viongozi mbalimbali wa CHADEMA

SAM_2974

SAM_2955   Mh Lema akiwajibika jukwaani hapo jana

SAM_2998 Millya akifuatilia hotuba za wenzake kwa umakini ka anavyoonekana

SAM_3015 Zoezi la kupokea wananchama wapya likiendelea

SAM_2936

SAM_2988  Magari mapya ya CHADEMA maalumu kwa shughuli za kueneza ujumbe wa vuguvugu la mbadiliko. Gari hili na mengine ndiyo yalitumiwa na waliosafiri kwa barabara kwenda Mirerani tokea Arusha mjini.

SAM_2795Hawa nao walilazimika kukwea juu ya mti huu ili kuweza kushuhudia kila kitu kwa uzuri zaidi

SAM_2789  Kamera yetu iliweza kunasa taswira ya jengo la Mahakama ya Mwanzo Mirerani kama linavyoonekana pichani. Picha ya chini ni ofisi nyingine za kiserikali katika eneo hilo.

SAM_2792

SAM_2814  Mwananchi huyu mwanchama wa CCM, akiwa kazini jirani na eneo la mkutano nae alikuwa kivutio kwa makaamnda wa chadema hasa pale aliposimamia msimamo wake kwamba kwa namna yeyote ile hawezi kuhama CCM na kujiunga na CHADEMA. Pamoja na makelele yote lakini yeye aliweza kuendelea na kazi yake bila usumbufu.

Picha zote na Nuru Ndosi

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO