Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Obama asifu Senegal kwa demokrasia

Obama anatarajiwa kwenda Afrika Kusini kisha Tanzania kwa ziara yake ya pili Afrika

Rais wa Marekani Barack Obama ambaye yuko katika ziara yake ya Afrika, amesifu nchi ya Senegal kwa kuwa moja ya nchi zenye demokrasia thabiti barani Afrika.

Akiwahutubia waandishi wa habari nchini Senegal kwa mkondo wake wa kwanza wa ziara yake Afrika,baada ya mazungumzo na rais Macky Sall, Bwana Obama alisema kuwa Senegal iliandaa uchaguzi huru na wa haki pamoja na kuwa na kipindi salama cha mpito.

Pia aliisifu kwa kuwa na mtindo wa kusuluhisha migogoro kwa mazungumzo na mashauriano, wala sio kwa njia ya ghasia.

Alisema kuwa Afrika kama bara limepiga hatua kubwa upande wa demokrasia katika miaka ya hivi karibuni.

Obama atazuru Afrika Kusini ambako rais mstaafu Nelson Mandela anaugua sana na amelazwa hospitalini.

Aliwaambia waandishi wa habari kuwa wanamuombea Mandela pamoja na familia yake.

BBC Swahili


Rais Barack Obama (kushoto) na rais wa  Senegal  Macky Sall wakipeana mikono mara baada ya kuongea na wandishi wa habari rais  Obama akiwa katika ziara ya kutembelea nchi za  Senegal, Africa ya kusini na Tanzania

Wananchi wa wa Senegal wakiwa barabarani wakimsubiri rais Obama pamoja na rais wa senegal  Sall wakiwa mitaa ya huko leo

Rais Baraka Obama akiwapungia baadhi ya watu waliokuja kumsikiliza wakati akiongea na wandishi wa habari leo nchini Senegal kulia ni rais Macky Sall mkutano uliofanyika katika jengo la ukulu ya Dakar,

PICHA ZAIDI MPOKEZI YA RAIS OBAMA NA MKEWE NCHINI SENEGAL

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO