Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Udiwani Makuyuni: Joshua Nassari wa Chadema Apigwa na Kuumizwa Katika Zoezi la Kupiga Kura Hadi Kukimbizwa Hospitali ya Seliani Jijini Arusha

DSC09368

DSC09369

Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Mh Joshua nassari akimueleza mmwenyekiti wa Chadema taifa Mh Freeman Mbowe aliyekwenda kumjulia hali alipolazwa katika hospitali ya Selian ya jijini Arusha alikolazwa mchana wa leo baada ya kupigwa sana na wananchi wanaoaminika kutoka kwa wapinzani wa Chadema  katika kinyang’antyiro cha kuwania Udiwani wa Kata ya Makuyuni-Monduli uliofanyika leo.

Katika ziara hiyo hospitalini hapo, Mh Mbowe aliongozana na Mbunge wa Arusha Mjini pamoja na James ole Millya.

Aidha taarifa kutoka Makuyuni zinaeleza kuwa uchaguzi wa leo ulitawaliwa na matukio ya kushambulia watu wa Chadema wakiwemo mawakala wanaosimamia uchaguzi huo kuwakilisha Chadema, na inadaiwa kuwa kuna wakala mmoja amepigwa na kuumizwa vibaya mkono wake.

Mawakala wa Chadema walilazimika kukimbia kuacha vituo vya uchaguzi kuokoa maisha yao.

Kupigwa kwa Nassari kama wakala mkuu wa Chadema katika Kata hiyo kumeelezwa na mwenyekiti wa chama hicho kuwa kutaathiri matokeo ya uchaguzi huo hasa ya Chadema.

Blog hii ilizungumza na kiongozi mmoja wa Chadema akaieleza kuwa kwa kitendo cha wawakilishi hao wa Chadema kupigwa kunamaanisha kuwa uchaguzi huo ni batili kayika mazingira na hali halisi.

IMG-20130616-WA0003

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO