Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Taswira: Baadhi ya Matukio Mbalimbali Katika Mikutano ya Kampeni za Udiwani za CHADEMA Kata za Themi, Kimandolu na Kaloleni kwa Juma Hili Linaloishia Leo

Kata ya Kaloleni

DSC07092Mbunge wa Arusha Mjini na Mjumbe wa Kamati Kuu Chadema, Mh Godbless Lema akihutubia mamia ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni za chama hicho kuwania Udiwani wa Kata ya Kaloleni, mkutano uliofanyika eneo la Ekenya (mashariki ya uwanja wa Sheikh Amri Abeid) siku ya Mei 30, 2013. Katika Mkutano huo Lema aliainisha ufisadi mkubwa wa jumla ya sh 12 bilioni uliofanywa na watumishi wa Halamshauri ya Manispaa ya Arusha akirejea taarifa ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka unaoishia 2012, ikiwemo kutowasilishwa kwa makusanyo ya ushuru mbalimbali na matumizi mengine kukosa nyaraka za kuthibitisha matumizi yake.

DSC07087

DSC07097

DSC07091Umati wa wananchi na baadhi ya viongozi katika mkutano huo


Themi Relini

DSC07135Katibu wa Chadema Wilaya ya Arusha Mjini, Martin Sarungi (kulia) akiwa na Mgombea wa Chadema Kata ya Themi, “Kabouru” (katikati) katika mkutano wa Kampeni eneo la Relini uliofanyika Mei 31, 2013

DSC07147Diwani wa Chadema Halmashauri ya Moshi, Mh Hawa Ali akiwa jukwani kuhutubia wananchi waliojitokeza katika mkutano huo

DSC07139Kiongozi wa Vijana wa Chadema Korogwe na Mjumbe wa Baraza la Kanda ya Kaskazini Chadema, Bi Aminata nae alipata wasaa wa kuzungumza mkutanoni hapo

DSC07163Huyu ni Anrose, mwana mama ambaye ana nia ya kuwania Ubunge mwaka 2015 katika Jimbo analoongoza Mh Lyatonga Mrema (TLP) kwa sasa.

DSC07142Kiongozi wa Vijana Chadema Wilaya ya Hai, Mss Doris Cornel akifafanua jambo mkutanoni hapo

DSC07171Diwani wa Kata ya daraja Mbili, Mh Msofe nae alikuwepo mkutanoni hapo kumnadi mgombea wa Chadema

DSC07160Mjumbe wa Halmashauri ya Mji Mdogo wa Usa River, Arumeru Mashariki Mh Josephine Annaely akisisitizia umuhimu wa wananchi kutumia fursa ya kupiga kura waliyoipata kwa manufaa yao kwa kuchagua viongozi wanaofaa

DSC07166Mwenyekiti wa Vijana wa CHADEMA WIlaya ya Arusha Mjini, Noel Olevaroya akihutubia. Nole alitumia nafasi hiyo kukemea vikali matendo ya baadhi ya wanasiasa wanaohubiri udini na ukabili kwa nia ya kuwagawa watanzania ili wawatawale ama wapate manufaa yao kisiasa, na kudai kwamba hali hiyo ikiachwa iendelee italeta kadhia ambayo hakuna mtu atakayekuwa salama na watanzania hawataulizia tena dhahabu na mali zao viko wapi.

DSC07173Mgombe mwenyewe wa Udiwani Kata ya Thei kupitia Chadema kimwaga sera zake

DSC07179Bossi mzito wa Arusha255 akibadilishana mawazo na waheshimiwa madiwani na vicheko vya hapa na pale mkutanoni hapo


Kata ya Kimandolu

DSC07182_thumbMpiga Kampeni mkuu wa mgombea wa Chadema Kata ya Kimandolu Bw Derick Magoma akimnadi mgombea wake Mch Rayson Ngowi katika mkutano uliofanyika jana jirani na City Link Hotel, Kimandolu.

DSC07104_thumbMgombea wa Chadema Kata ya Kimandolu Mch Rayson Elishadai Ngowi akijinadi kwa wapiga kura katika mkutano wa kampeni zake uliofanyika eneo Pride Msikitini-Kimandolu tarehe 30 Mei, 2013

DSC07106_thumbMeneja Kampeni wa mgombea wa Chadema Kata ya Kimandolu..Bw Magoma Derick Magoma (mwenye suti) akitafakari jambo katika jukwaa la viongozi wakuu

DSC07118_thumbMgombea wa Chadema Kata ya Kimandolu Mch Rayson Nowi akisalimina na mdau wake huku bosi wa Arush255 akishuhudia

DSC07102_thumbBaadhi ya wananchi wakifuatilia mkutano huo uliofanyika Pride, Kimandolu. Picha zote na SeriaJr

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO