Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Taswira: Wabunge wa Chadema Wateka Viwanja Vya Mahakama Kuu Arusha Leo Wakiwasubiri Kina Lissu Kupandishwa Kizimbani, Hata hivyo hawakupelekwa Mahakamani!

P1020702Mbunge wa Rombo (CHADEMA) Mh Joseph Selasini akitoa ufafanuzi wa taarifa kuhusu wabunge wenzake waliokuwa wameshikiliwa na Polisi jana kuachiwa kwa dhamana ya Polisi asubuhi ya leo bila kufikishwa Mahakamani kama ambavyo walitarajia.Selasini alikuwa akizungumza na watu waliokuwa wamejiandaa kuwadhamini wenzao takribani 70 waliokamatwa jana sambamba na wabunge, Tundu Lissu, Joyce Mukya, Mustafa Akoonay na Mzee Said Arfi.

P1020700

Mbunge wa Jimbo la Ubungo anaesimimia Kurugenzi ya upashanaji habari na sera wa Chadema, Mh John Mnyika akitoa taarifa na msimamo wa chama juu ya maziko ya kiongozi wao aliyekufa kwenye bomu Jumamosi na alichodai kuwa ni njama za CCM kutaka kuharibu ushahidi ama kuwatorosha mashahidi walioshuhudia wanaodaiwa kuwa askari ambao waliwapiga kwa risasi na baadhi wakidai walimuona mipuaji bomu na sare za jeshi hilo.

Mnyika amesema kwasababu Jeshi la Polisi limedhamiria kuhakikisha marehemu huyo hataagwa kwenye eneo lolote la wazi kwa mikutano Jijini hapa, basi Chadema wameamua kwa maafikiano na familia ya wafiwa kwamba marehemu ataagwa Kanisani na mazishi yake yatafanyika hapa Arusha eneo ambalo litatajwa baadae.

P1020718Mwanasheria Mabere Marando akifafanua jambo kwa Mh John Mnyika katika viwanja vya Mahakama Kuu Kanda ya Arusha leo. Wanaoshukudia ni Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Mh mani Golugwa (katikati) pamoja na afisa wa chama makao makuu.

DSC09422Wabunge wa Chadema, Grace Kiwhelu (katikati) na Vicent Kiboko Nyerere (kushoto) wakiwasili katika viwanja vya Mahakama

DSC09425Mbunge wa Kawe, Mh Halima Mdee akiwasili Mahakamani hapo

P1020687Jihn Mnyika akibadilishana mawazo na watu wa Arusha katika viwanja vya Mahakama hii leo

P1020645Wabunge wakipiga stori. wanaotazama mbele, kutoka kushoto Vicent Nyerere, Joseph Selasini, Mh Akoonay na Ezekia Wenje

P1020648

P1020654Mbunge wa Rombo akiongea na waandishi wa habari na kutoa masikitiko yake kwa kitendo alichodai kushuhudia kwa mara ya kwanza kwa askari Polisi kuyapia na kuhabiru magari na pikipiki za raia.

P1020658Wabunge wa Chadema wakiongozwa na Mh Selasini wakiwa na furaha

P1020662Mh Selasini, Mh Wenje, Mh Nanyaro na waau wengine wakifurahia jambo mahakamani hapo

P1020666Wakili Marando, Katibu wa Kanda ya Kaskazini Chadema Amani Golugwa na maofisa wa Chadema makao makuu wakiwasili viwanja vya Mahakama

P1020689

Mbunge  wa Kawe Halima Mdee, Mwenyekiti BAVICHA, Jihn Heche, Mwenykiti Vijana Arumeru Mashariki Methew Kishili na Bossi Mzito wa Arusha255 wakipiga stori mbili tatu katika viwanja hivyo

P1020694Kijana huyu alikuwa akizungumza na waandishi wa habari na kuelezea wasiwasi wa maisha ya pacha mwenzake ambaye amelazwa hospitali ya Seliani kufuatia kuumia katika mlipuko wa bomu jumamosi na sasa anafuatiliwa na maaskari kanzu hospitalini wanaodaiwa kuvaa majoho ya madaktari kwa nia ya kutaka kumtorosha ndugu yake ambaye ameelezwa kushuhudia kila kitu wakati bomu likirushwa hadi anapigwa risasi na mtu aliyevalia nguo za kiaskari.

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO